Mwenyekiti
 Taifa wa Chama Cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahimu Lipumba akizungumza
 na waandishi wa Habri jijini Dar es Salaam jana wakati akitoa tamko la 
kulaani kwa kitendo cha Naibu Spika wa Bunge la Muungano wa Tanzania, 
Job Ndugai kuwanyanyasa na kuwazalilisha Wabunge wa upinzani akiwepo 
Kiongozi wa Kambi rasmi ya upinzani Bungeni, Freeman Mbowe. Picha na 
Venance Nestory 
…………………………………………………………………………………
Dar 
es Salaam. Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim 
Lipumba ameitaka Serikali kutafuta ufumbuzi wa haraka wa matatizo ya 
kiuchumi, kwa kuwa hali ilivyo sasa ni mbaya.
Profesa Lipumba ambaye pia ni 
profesa wa uchumi alisema hivi karibuni Dar es Salaam kuwa hali ya 
uchumi imezidi kudorora na kusababisha maisha ya wananchi wengi kuwa 
magumu.
“Vijana wa siku hizi wengi 
hawana simile kushughulika na mambo yanapokwenda sivyo, ajabu ni kwamba 
wanaofanya mambo hayo yawe magumu wamekuwa wepesi wa kutetea kwa hoja 
zisizo na msingi kwa masilahi yao binafsi,” alisema.
Akizungumzia maazimio 
yaliyofikiwa kwenye Kikao cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la CUF 
kilichofanyika Desemba 21-22 mwaka huu Dar es Salaam, alisema hatua ya 
kupandishwa kwa gharama za umeme iliyotangazwa hivi karibuni na Shirika 
la Umeme Tanzania (Tanesco) ni miongoni mwa mambo ambayo yanaendelea 
kuongeza ugumu wa maisha kwa wananchi, jambo ambalo lingeweza kuzuilika 
kwa shirika hilo kudhibiti wizi wa nishati hiyo.
Kuhusu hali ya kisiasa nchini, 
Profesa Lipumba alisema Baraza Kuu limetoa wito kwa vyombo vya Dola kuwa
 na weledi na uadilifu na kuacha kutekeleza amri za wanasiasa zisizojali
 utawala wa sheria na haki za binadamu ili vipunguze uhasama baina yao 
na raia.
“Serikali pia isitumie Jeshi la 
Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika kushughulikia masuala ya uvunjifu wa 
sheria katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu, badala yake kazi hiyo 
ifanywe na Jeshi la Polisi kwa mujibu wa taratibu za kisheria. Nao pia 
waongezewe uwezo wa kiutendaji,” alisema.
Alisema
 CUF inaona si vyema kutumia JWTZ kudhibiti vurugu kwa kuwa wanajeshi 
hao hawana mafunzo ya kukamata wananchi wenye tuhuma za uhalifu 
isipokuwa wamefundishwa jinsi ya kulinda usalama wa nchi katika mipaka.
CHANZO: MWANANCHI

No comments:
Post a Comment