RC Iringa Dr Christine Ishengoma
Mkuu
 wa mkoa  wa  Iringa  Dr Christine  Ishengoma ametuma  salama  kali za  
Krismas na Mwaka  mpya kwa   wafanyabiashara  watakaopandisha bei  ya  
vyakula msimu  huu wa sikukuu kuwa watachukulia hatua  kali.
Huku 
 akiwataka wakurugenzi  wa Halmashauri  zote za wilaya ,wakuu wa wilaya 
,maofisa  biashara  wa  wilaya  na mkoa huo  kuanza  kuzunguka mitaani  
kuchunguza  bei ya  bidhaa na  kuwataka kuchukua hatua kwa  wote  
wanaliopandisha  bei kiholela.  
Akizungumza
 na  wanahabari jana  ofisini  kwake  ,mkuu  huyo wa mkoa alisema  kuwa 
imekuwa ni kawaida kwa baadhi  ya  wafanyabiashara  kutumia  sikukuu 
mbali mbali  kujipatia fedha  kwa kuwanyonya wananchi jambo ambalo 
katika mkoa huo halitavumiliwa kamwe. 
Alisema 
 kuwa  lengo  la  serikali  ya  mkoa kuwabana  wafanyabiashara ni 
kutaka  kuona  wananchi  wanasherekea  sikukuu  hizo   na kununua 
vyakula na vitu  mbali mbali  vya sikukuu kulingana na bejeti  
waliyoitenga  kwa  sikukuu  hizo. 
”
 Serikali  ya  mkoa haitakubali  kuona  wananchi  wakiibiwa kwa kuuziwa 
vyakula kwa bei   kubwa za  sikukuu….tumejipanga  kuchukua hatua  kali 
na tunaomba  wananchi pia  kutoa ushirikiano “
Hata 
 hivyo mkuu  huyo wa mkoa alivipongeza  vyomba vya  habari  mkoani 
Iringa kwa mchango  mkubwa  wa kuhamasisha maendeleo   na kutaka  
kuonyesha  ushirikiano katika wakati  huu wa sikukuu kwa  kufanya  
uchunguzi  wa  wafanyabiashara  wanaopandisha  bei.
Katika hatu nyingine mkuu huyo wa mkoa aliwataka wakulima kutumia mvua zinazoendelea kunyesha kwa kupanda mazao mbali mbali yakiwemo yale yanayohimili ukame kwa maeneo yeye changamoto ya mvua.
Katika hatu nyingine mkuu huyo wa mkoa aliwataka wakulima kutumia mvua zinazoendelea kunyesha kwa kupanda mazao mbali mbali yakiwemo yale yanayohimili ukame kwa maeneo yeye changamoto ya mvua.
Pia 
 aliwataka  maofisi  kilimo na  mabwana shamba  kuachana na mpango  wa 
kuvaa suti na  kushinda maofisini wakati  huu wa msimu wa kilimo badala 
ya kwenda  kuwaelimisha  wakulima .
Dr 
 Ishengoma  aliwataka  wakulima  kuendelea  kutumia mbolea  ya Minjingu 
ambayo  alidai hata  yeye  amekuwa akiitumia na ni miongoni mwa mbolea  
bora nchini na kuwataka  kuepuka maneno ya kukatisha tamaa 
yanayoendelea  kutolewa na  watu juu ya mbolea  hiyo.
Wakati 
 huo huo  serikali  ya  mkoa  wa Iringa imepiga marufuku  wazazi 
kuwaruhusu watoto  wao kwenda  kushiriki madisco toto  ambayo alidai ni 
hatari  na ni  vema  wazazi na walezi wa watoto mkoani Iringa  kuwa 
makini na kuachana na tabia ya  kuwaacha  watoto  wao peke  yao wakati  
huu wa sikukuu.
.jpg)
No comments:
Post a Comment