TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, December 22, 2013

MANJI AMKINGIA KIFUA KASEJA, ASEMA SIMBA KUMTUNGUA MATATU SIO KIGEZO CHA KUSHUSHA THAMANI YAKE!!


KASEJA32 
Juma Kaseja `Tanzania One` amekingiwa kifua na bosi wake ,Yussuf Manji baada ya kufungwa mabao matatu jana kwenye mechi ya Nani Mtani Jembe

MWENYEKITI wa klabu ya Yanga, Yussuf Manji amemkingia kifua mlinda mlango wao mpya, Juma Kaseja baada ya kufungwa mabao matatu jana akiwa langoni katika mchezo wa Nani Mtani Jembe dhidi ya watani zao wa jadi, Simba Sc ambao Mnayama alishinda 3-1.
Mbao ya Simba sc katika mechi ya jana yalifungwa na Amis Tambwe aliyepiga mawili na kiungo Juma Awadh Issa, wakati la Yanga lilifungwa na Emmanuel Okwi.
Akizungumza leo na waandishi wa habari, Manji amasema hawakumsajili Kaseja kwa ajili ya kuifunga Simba SC, bali malengo yao ni kupata msaada wake katika michuano mikubwa ya soka barani Afrika.
Baada ya Yanga kufungwa jana, huku Kaseja akiwa langoni, katibu mkuu wa baraza la wazee la klabu hiyo, Mzee Ibrahim Akilimali, iliulaumu uongozi kwa kusema kuwa  usajili wa kipa huyo ni makosa na hauna baraka zao.
Manji amejibu mapigo na kueleza kuwa umri unazidi kumtupa mkono mzee Akilimali  kwani ameshindwa kukumbuka kuwa , huyo Ivo mwenyewe aliondoka Yanga akiwa anatumikia adhabu ya kufungiwa miezi sita na uongozi wa wakati huo kwa tuhuma za kufungisha kwenye mechi dhidi ya  Simba SC.
Pia Manji alihoji wakati Simba ikisawazisha mabao yote matatu  katika mchezo wao wa ligi kuu soka Tanzania bara oktoba 20 dhidi ya Simba sc , Kaseja alikuwa langoni?.
Mwenyekiti huyo alisema  si jambo zuri kulaumiana pale yanapotokea makosa, bali ni kuwa na mshikamano kwa ajili ya maendeleo ya Yanga.
“Tunaheshimu uwezo wa Kaseja, thamani yake ni kubwa. Hakuna kipa yeyote nchini aliyedaka mechi nyingi za kimataifa kama kipa huyu. Kamwe hatuwezi kumshusha thamini yake na uwezo wake kwa kufungwa mabao matatu kwenye mechi ya jana ambayo ilikuwa sawa na bonanza tu”. Alisema Manji.
Manji alisema mechi ya jana walicheza kumfurahisha mdhamini wao, TBL, lakini haikuwa na maana yoyote na matokeo ya kufungwa wala hayajawaingia akilini.
Hata hivyo Manji amewapongeza Simba SC kwa kucheza soka safi, hivyo walistahili ushindi katika mchezo wa jana.
 Kuelekea ngwe ya lala salama ya ligi kuu na michuano ya Kimataifa , Manji alisema wataboresha timu pamoja na benchi la ufundi  kwa tafsiri ya kuwaondoa makocha wao Ernie Brandts na wasaidizi wake, Mzawa Fredy Felix Minziro na Mkenya, Mkenya Razack Ssiwa 
“Timu itaenda tena Ulaya kuweka kambini kama walivyofanya waka jana. Naamini tutajivua vizuri na kuwa makali zaidi kutetea ubingwa wetu na kufanya vizuri michuano ya kimataifa”. Alisema Manji.
Ili kuongeza makali, Yanga imesajili wachezaji watatu katika dirisha dogo la usajili ambao ni mlinda mlango, Juma Kaseja, kiungo Hassan Dilunga na mshambuliaji mahiri raia wa Uganda, Emmanuel Anord Okwi.
Wachezaji hao walitumika jana, lakini hawakufua dafu mbele ya kikosi cha Simba Sc kilichoonekana kuwa bora zaidi Yanga.

No comments:

Post a Comment