MAANDALIZI
 ya kombe la Mapinduzi linalotarajia kuanza kutimua vumbi januari mosi 
mwakani yanakwenda vizuri na timu zote zilizothibitisha kushiriki 
zinatarajia kuwasili desemba 31 mwaka huu.
Msemaji
 wa kamati ya mashindano , Farouk Karim amesema kuwa timu za Tusker fc, 
AFC Leopard za Kenya, KCC, URA za Uganda , Simba sc, Yanga, Azam fc na 
Mbeya City za Tanzania bara tayari zimeshathibitisha kushiriki na kamati
 ya maandalizi imeshakamilisha  taratibu za kuzipokea.
SIMBA
 imepangwa kufungua pazia la michuano ya Kombe la Mapinduzi kwa kucheza 
na AFC Leopards ya Kenya Januari Mosi wakati Yanga wakishuka dimbani 
siku inayofuata kuikabili Tusker FC.
kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Italia, Cesare Prandelli.
Karim
 amesema mgeni rasmi katika mechi ya ufunguzi itakayopigwa januari mosi 
majira ya saa mbili usiku katika uwanja wa Aman kisiwani Unguja baina ya
 Simba sc dhidi ya AFC Leopard ya Kenya atakuwa kocha mkuu wa timu ya 
Taifa ya Italia,  Cesare Prandelli.
Pambano
 la Simba na Leopards litatanguliwa na mechi kati ya wenyeji KMKM na KCC
 ya Uganda litakalopigwa saa 10 jioni kwenye uwanja huohuo.
“Ninavyozungumza
 na wewe muda huu, Prandelli yupo hapa Zanzibar mapumzikoni na tayari 
amekubali kufungua michuano hii yenye maana kubwa katika miaka 50 ya 
mapinduzi ya Zanzibar”. Alisema Karim.
Kikosi cha Simba sc
Karim alisema katika michuano ya mwaka huu viwanja viwili vitatumika ambavyo ni Gombani kisiwani Pemba na Aman Kisiwani Unguja.
“Uwanja
 wa Gombani upo katika hali nzuri na unavyojua una nyasi za bandia. 
Uwanja wa Aman umefanyiwa ukarabati mkubwa na hivi sasa wataalamu kutoka
 China wapo hatua za mwisho kabisa kukamilisha shughuli yao”. Alisema 
Karim.
Mratibu
 huyo alitoa wito kwa wadau, wapenzi wa soka visiwani Zanzibar 
kujitokeza kwa wingi kwani kamati ya mashindano inategemea mapato ya 
milangoni kufanikisha mipango.
“Michuano
 hii inagharimu zaidi ya shilingi milioni 600, hatuna fedha hizo, 
tunategemea mapato ya milangoni, hivyo mashabiki kufika kwao  kwa wingi 
ndio mafanikio yetu”. Aliomba Karim.
AFC Leopard
Aidha
 ameziomba taasisi na makampuni ya bara na visiwani kujitokeza kufanya 
matangazo katika michuano hiyo ili angalau wapate pesa za kuendeshea 
michuano hiyo.
Michuano
 iliyopita, Azam fc walitwaa ubingwa, lakini mwaka huu kuna changamoto 
mpya hasa kutokana na uwepo wa timu za Dar Young Africans na Mbeya City 
ambazo hazikushiriki.
Mechi
 zote za hatua ya makundi na robo fainali zitafanyika kwenye viwanja wa 
Gombani Pemba na Aman Unguja, wakati nusu fainali na fainali zitapigwa 
kwenye Uwanja wa Aman.
Katika
 michuano iliyopita Simba waliishia nusu fainali baada ya kuondolewa na 
Azam FC kwa mikwaju ya penalti 5-4 baada ya mechi kumalizika kwa sare ya
 2-2 hata baada ya kuongezwa dakika 30.



No comments:
Post a Comment