TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 28, 2013

WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA WATANGAZWA

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Jumanne Sagini, akifafanua jambo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo (jana), kuhusu wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka 2014. Kushoto ni Naibu wake, Zuberi Samataba. (Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Jumanne Sagini, akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo (jana) kuhusu wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka 2014. Kushoto ni Naibu wake, Zuberi Samataba.
Baadhi ya waandishi wa habari, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Jumanne Sagini, jijini Dar es Salaam leo (jana), wakati alipozungumza nao kuhusu wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka 2014. 
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Jumanne Sagini, akifafanua jambo wakati wa mkutano huo na waandishi wa habari, Dar es Salaam 
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Jumanne Sagini, akielezea jambo wakati alipokuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari, kwenye mkutano huo.
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Jumanne Sagini, akifafanua jambo waandishi wa habari, katika mkutano huo, jijini jana
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Jumanne Sagini, akisikiliza maswali ya waandishi wa habari, wakati wa mkutano huo na waandishi jijini, Dar es Salaam 
Na Magendela Hamisi
IDADI ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwakani umeongezeka kwa asilimia 31.37, huku ufaulu ukiongezeka kwa asilimia 19.
Hayo yalielezwa leo, jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Jumanne Sagini, wakati akitangaza wanafunzi waliomaliza darasa la saba ambao wamechaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Januari mwakan
Hata hivyo wakati idadi hiyo, ikifanikiwa kuchaguliwa kujiunga kidato cha kwanza, wanafunzi 13 matokeo yao yamefutwa kutokana na kubainika kufanya udanganyifu wakati wa mtihani huo kumaliza elimu ya msingi mwaka huu.
Kuhusu ufaulu kuongezeka Sagini alisema kwa asilimia 19 kutokana na watahiniwa 844,938 sawa na asimilia 97.34 waliofanya mtihani huo.
Alisema kati ya hao wasichana walikuwa 446,115 sawa
na asilimia 97.85 wakati wavulana ni 398,823 sawa na
96.78.Wanafunzi  23,045 sawa na asilimia 2.66 hawakufanya mtihani kwa sabanu mbalimbali ikiwemo ugonjwa, vifo na utoro.
“Matokeo hayo ya mtihani huo wa kumaliza elimu ya msingi yanaonesha alama ya juu ufaulu kwa wavulana ni 244 na wasichana ni 241 kati ya 250,” alisema.
Aliongeza kutokana na ongezeko hilo la ufaulu wanafunzi
411,127 kati ya 427,609 waliofaulu wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule za Serikali katika awamu ya kwanza ikiwa ni sawa na asilimia 96.15.
Alifafanua wanafunzi hao waliochaguliwa wasichana ni  201,021 na wavulana wakiwa 210, 106 huku akifafanua kuwa wanafunzi 6,482 ambao wamekosa nafasi awamu ya kwanza halmashauri zimetakiwa kukamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa 412 ili kufanikisha wanafunzi hao kujiunga na elimu ya sekondari kuanzia Februar na Machi mwakani.
Alitumia nafasi hiyo, kuitaja mikoa ambayo wanafunzi wake wamekosa nafasi za kujiunga kidato cha kwanza katika awamu ya kwanza ni  Morogoro wanafunzi 315, Katavi 261, Dar es Salaam 11, 796,  Dodoma 549, Mtwara 120, Mbeya 1484 na Geita 1578.
Aliwataka wazazi washirikiane na halmashauri kutatua tatizo hilo ili kutoa fursa kwa watoto waliochaguliwa kwenda shule.
Hata hivyo, alisema wanafunzi 13 wamefutiwa mitihani yao kutokana na kufanya udanganyifu na kwamba idadi ya udanganyifu kwenye mtihani huo imepunguaikilinganishwa na mwaka jana ambapo waliodanganya walikuwa 219.
CHANZO:  www.bayana.blogspot.com

No comments:

Post a Comment