TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, December 22, 2013

KAMISHNA WA SHERIA NA UENDESHAJI WA MAGEREZA AFANYA ZIARA YA KIKAZI MAGEREZA MKOA WA MANYARA

image (7)
Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akisalimiana na baadhi ya Maafisa wa Jeshi la Magereza toka Magereza mbalimbali ya Mkoani Manyara mapema leo (jana) Desemba 21, 2013 alipowasili katika Ofisi za Magereza Mkoa wa Manyara tayari kwa ziara ya Kikazi ya siku mbili.image (8) Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa pili kushoto) akiongea na baadhi ya Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza wa Mkoani Manyara(hawapo pichani) leo (jana) Desemba 21, 2013. Watatu toka kulia ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Manyara, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Bether Minde.image (9)  
Baadhi ya Askari wa Jeshi la Magereza toka Vituo mbalimbali vya Magereza Mkoa wa Manyara wakimsikiliza Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(hayupo pichani) wakati Baraza Maalum la Askari lililofanyika katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Magereza, Mkoani Manyara leo (jana)  Desemba 21, 2013.image (10) 
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Manyara, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Bether Minde akiwa ameongozana na Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(kushoto) wakati wa kutembelea baadhi ya maeneo mbalimbali ya Gereza la Mahabusu la Babati
(picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

No comments:

Post a Comment