TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, December 23, 2013

HAFRA FUPI YA SHIRIKISHO LA NGUMI ZA RIDHAA TANZANIA KWA AJILI YA KUHAMASISHA MCHEZO WA NGUMI KWA VIJANA TANZANIA

 Baadhi ya wachezaji wa timu ya Taifa wa ngumi za Ridhaa pamoja na wadau wengine wa mchezo huo katika Picha ya pamoja, wakati wa hafra hiyo
 Aliyesimama kushoto ni mkurugenzi wa Afrika Mashariki kupitia kinywaji cha Battery Bwana Tony Misokia akiwa anaongea na wananchi walioshiriki katika Hafra hiyo.
 
 Kutoka kushoto ni Makamu wa Rais wa Shirikisho la Ngumi za ridhaa Tanzania (BTF) Bwana. Lukelo  Anderson akiwa sambamba na Afisa habari wa Ngumi za ridhaa Tanzania  Bwana Salum Viduka wakati wa Hafla hiyo.
 Hawa ni Baadhi ya wachezaji wa  Shirikisho la Ngumi za ridhaa Tanzania (BTF)
 Wa kwanza kulia ni Nahodha wa Timu ya Taifa ya Ngumi za ridhaa Tanzania bwana Nassari Mafuru
 Kutoka kushoto aliyevaa shati jeupe ni Bwana Anthon Mwang’onda ambaye ni mjumbe wa mashindano na vifaa wa Shirikisho la Ngumi za ridhaa Tanzania (BTF) akiwa na Kocha Mkuu wa timu ya Taifa Bwana Hassan Mzonge
Shirikisho la ngumi za ridhaa Tanzania  limefanya hafla fupi iliyojumuisha wachezaji wa ndondi , makocha wadau na Vyombo vya habari kwaajili ya kuendeleza  mshikamano wa kuweza kuwainua vijana ambao bado
hawajaweza kupata ajira  kujiunga na shilikisho la ngumi za ridhaa Tanzania
Shilikisho hilo ambalo limeanzisha mashindano ambayo yanatambulika kwa jina la  PSPF  Boxing Award sambamba na wadhamini wa mashindano hayo waliandaa hafla hiyo  iliyofanyika katika eneo la   (CnG) ambapo waliweza kudhamini kwa kuandaa chakula cha usiku kwaajili ya kuendelea kuweka mahusiano baina ya washiriki wote wanao shiriki katika kuendeleza mchezo wa ngumi Tanzania
Akizungumzia lengo la kuweka hafla  hiyo Afisa habari wa shirikisho la ngumi Tanzania Bw.Salum Kuhowa Viduka amesema “Tunawaomba wanajamii kuweza kutupa ushirikiano kwa muda wote ambao mashindano haya  huwasili katika miji,wilaya, manispaa, nk kuweza kujitokeza kwa wingi ili kuona jinsi fursa kwa vijana zinavyo patikana kupitia mchezo wa ngumi za Ridhaa”
Mwisho Makamu Rais  Bw.Lukelo Andason aliweza kufunga hafla hiyo kwa kuwapongeza watu wote walio weza kufika na kujumuika pamoja ili kuendeleza kujenga umoja wa ngumi Tanzania.

No comments:

Post a Comment