TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, December 26, 2012

Dk. Mukangara atembelea vijiji vya kitigiri na Bugalama wilayani Geita


 
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara  (kulia) akimsikiliza Mwenyekiti wa kikundi cha Nyakalalo kililopo  kijiji cha Kitigiri wilayani Geita, Gideon Msabila (kushoto)  ambaye alimuelezea jinsi walivyonufaidika na mkopo wa mfuko wa maendeleo ya vijana fedha ambazo zimewawezesha kufungua duka  la rejareja la bidhaa za nyumbani.
  Picha na Anna Nkinda – Maelezo
 
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara  (kulia) akimsikiliza Mwenyekiti wa kikundi cha Bodaboda kilichopo kijiji cha  Bugalama  wilayani Geita,  Enos Komanya  wakati alipotembelea kikundi hicho ambacho kilipata mkopo  kutoka mfuko wa maendeleo wa halmashauri. Waziri Dk. Mukangara  alitembelea kijiji hicho jana ili kuona fedha za mkopo zilizotolewa na mfuko wa maendeleo ya vijana zimewasaidiaje vijana kujikwamua kimaisha.
 
Vijana wa kikundi cha kusaidiana kulima cha Busaka katika kijiji cha Kitigiri wakifurahia fedha shilingi 50,000/= walizopewa jana na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara  (wanne kulia) kwa ajili ya kununulia soda za sikukuu ya Krismasi . Waziri Dk. Mukangara  aliwahimiza vijana hao kujiunga kwenye vikundi vya maendeleo vya kilimo ili weweze kupata mkopo wa kununulia pembejeo na kuweza  kuzalisha chakula kwa wingi zaidi.
 
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara  (wanne kulia) akiwa katika picha ya pamoja  na viongozi wa wilaya ya Geita, Kata ya Bukondo na  kijiji cha Kitigiri mara baada ya kumaliza ziara yake katika kijiji  hicho jana ili kuona fedha za mkopo za mfuko wa maendeleo ya vijana  zimewasaidiaje vijana kujikwamua kiuchumi.
……………………………………………………
Na Anna Nkinda – Maelezo, Geita
 Vijana  wametakiwa kushiriki katika suala la ulinzi na usalama wa maeneo wanayoishi kwa kujiunga na vikundi vya ulinzi shirikishi ili kulinda na kusimamia rasilimali za vijiji vyao.
Hilo litafanikiwa endapo vijana  watakuwa na moyo wa kujituma  na kutambua kuwa wanajukumu la kujenga taifa kwa kuhakikisha kuwa wanajiletea maendeleo yao na nchi kwa ujumla kutokana na  kazi mbalimbali wanazozifanya.
Rai hiyo imetolewa  mjini hapa jana  na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara  wakati akiongea kwa nyakati tofauti na wanavikijiji vya Bugalama na Kitigiri vilivyopo wilayani Geita alipozitembelea baadhi ya Vyama vya Kuweka Akiba na Kukopa (SACCOS) zilizopata mkopo  kupitia mfuko wa maendeleo wa vijana na fedha za maendeleo ya mfuko wa Halmashauri.
Dk. Mukangara alisema kuwa maendeleo ya nchi yanawategemea vijana ambao ndiyo nguzo ya taifa  hivyo basi wizara yake kupitia halmashauri za wilaya itahakikisha kuwa inatoa mafunzo ya kuwajengea uwezo vijana jambo la muhimu ni kujiunga katika vikundi vya maendeleo ili waweze kufikiwa kwa urahisi.  
“Uongozi wa kijiji uhakikishe kuwa  unawahimiza  vijana na kuwajengea  uwezo katika mtazamo wa kujitengemea, kujituma na kufanya kazi na  kujiunga kwenye vikundi vya maendeleo  ili iwe rahisi kupata mkopo kupitia SACCOS zilizopo vijijini mwenu” alisema Dk. Mukangara.
Aliwataka wanakijiji hao  kuwasimamia vijana wao ili wanawajibike na  kutambua  kuwa wanajukumu kubwa la kuhakikisha kuwa wanashiriki katika shughuli za kilimo cha chakula na biashara jambo ambalo litasababisha kuwa na chakula cha kutosha na kuepukana na janga la njaa.

No comments:

Post a Comment