TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, December 26, 2012

Upandishwaji vyeo katika jeshi la polisi ni wa kawaida, kigezo kikuu ni sifa

BAADHI askari wa kike wa Jeshi la Polisi nchini (WP), wameulalamikia uongozi wa jeshi hilo kutowapandisha  vyeo kwa muda mrefu tofauti na wenzao wa kiume ambao wamekuwa wakipandishwa mara kwa mara. 
Hatua hiyo imekuja baada ya askari hao kukutana mwishoni mwa wiki Jijini Dar es Salaam  katika kikao cha siri chenye lengo la kutafuta suruhisho la tatizo hilo.
Akizungumza kwa niaba ya wenzake jijini Dar es Salaam jana, mmoja wa askari hao, kwa sharti la kutotajwa jina, alisema suala la kutopandishwa vyeo limekuwepo kwa muda mrefu bila hatua zozote kuchukuliwa na uongozi wa jeshi hilo.
Alisema anastaajabishwa na utaratibu uliopo kwa sababu, licha ya kupewa mafunzo pamoja, bado wanagandamizwa pindi wanaporudi kwenye vituo vya kazi, ambapo askari wa kiume kupewa upendeleo wakupandishwa cheo haraka.
“Tunashangaa utaratibu huu utaisha lini, kwani sheria za jeshi letu zinasema kuwa askari yoyote wa kike au wa kiume anapaswa kupandishwa cheo baada ya muda mchache wa kumaliza mafunzo” alisema askari huyo.
Askari  huyo aliongeza kuwa endapo ikitokea askari wakike kupandishwa cheo kwa muda sitahiki, eidha ni kwa kujuana, ukabila na mkubwa fulani au kutoka kijiji kimoja.
Pamoja na hayo, aliivitaja baadhi ya vyeo ambavyo wamekuwa wakivilalamikia kutopewa  ni kama Msaaidizi wa polisi, Msaidizi wa Inspekta wa polisi, Inspekta wa Polisi, na vingine ambavyo wamekuwa wakitaka kupandishwa.
Kwa mujibu wa askari huyo, vyeo ambavyo vimekuwa vikitolewa kwa askari hao ni usajenti  na koplo ambavyo hukaa navyo hadi kustaafu kazi au kufariki.
Alipoulizwa  Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Advera Senso, ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Jeshi hilo, kuhusu nadai hayo, alisema mfumo wa upandishwaji vyeo katika jeshi hilo, ni wakawaida ambapo kigezo kuu ni sifa.
“Hakuna askari wakike wala wakiume bali wote ni askari na wako sawa kigezo kikubwa kinachoangaliwa katika upandishwaji vyeo hivyo ni sifa”alisema Senso 
Alisema mfumo wa jeshi hilo, unawachukulia kuwa askari wote kuwa wako sawa, pale inapotokea askari wakiwemo wanawake kama waana sifa zinazostahili kupandishwa cheo inafanyika hivyo na si vinginevyo.

No comments:

Post a Comment