TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 29, 2012

Tanzania haiwezi kukwepa maendeleo ya bioteknolojia ya utandawazi duniani

 
Naibu katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Eng. Ngosi Mwihava akifungua Warsha kwa maafisa wa mipakani kuhusu usimamizi wa mazao na bidhaa zitokanazo na Bioteknolojia ya kisasa. Kulia ni Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dkt. Julius Ningu na kushoto ni Afisa Mazingira Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi Esta Makwaia. Warsha hii imefanyika leo kwenye Hotel ya La kairo jijini Mwanza
 
Washiriki wa Warsha ya Usimamizi wa mazao na bidhaa zitokanazo na bioteknolojia ya kisasa wakiwa kwenye picha ya pamoja na mgeni rasmi (katikati) Mara baada ya kufungua warsha hiyo kwenye Hoteli ya La kairo Jiji Mwanza
 …………………………………………….
Lulu Mussa na Ali Meja
Mwanza
 Imeelezwa kuwa Tanzania kama nchi nyingine haiwezi kukwepa maendeleo ya bioteknolojia kutokana na utandawazi na maendeleo duniani kote, kwa kuwa bioteknolojia ya kisasa ni nyenzo muhimu katika kukuza uchumi na kupunguza umaskini, kuboresha kilimo, uzalishaji viwandani, afya na hifadhi ya mazingira.
 Hayo yamesemwa leo na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Eng. Ngosi Mwihava katika warsha ya siku moja kwa maafisa wa mipakani kutoka mikoa ya kanda ya ziwa, warsha iliyolenga kukuza uelewa kwa watendaji wanaosimamia mazao na bidhaa zitokanazo na bioteknolojia ya kisasa.
 Amesema, Serikali kwa kutambua mchango mkubwa unaoweza kupatikana kutokana na matumizi ya bioteknolojia ya kisasa katika sekta za afya, kilimo, viwanda na mazingira, imeridhia Itifaki ya Cartagena ya Mkataba wa Bioanuai mwaka 2003 kwa lengo la kuhifadhi mazingira kwa kuzingatia usalama katika usafirishaji,  kuunda na kupitisha mfumo wa kitaifa wa usimamizi wa matumizi salama ya Bioteknolojia mwaka 2007.
 Eng. Mwihava amewaasa watendaji katika maeneo ya mipakani kuwa na usimamizi madhubuti katika maeneo yao ya kazi kwa kuwa mipaka kati ya Tanzania na nchi nyingine ndiyo njia kuu za uingizaji wa mazao na bidhaa zitokazo nje.
 Pamoja na faida za bioteknolojia hiyo ya kisasa Eng. Mwihava amewataka watendaji hao kuwa makini na athari zinazoweza kutokana na matumizi ya teknolojia hiyo pale itakapotumiwa bila kufuata taratibu za usalama zilizowekwa.
 Warsha hii ya siku moja kwa imewashirikisha maafisa forodha, Maafisa Afya na watafiti wa Mazao kutoka Mikoa ya Mwanza, Mara na Kagera, kutoka Idara , wakala za Serikali na sekta binafsi.

No comments:

Post a Comment