Naibu
 katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Eng. Ngosi Mwihava akifungua Warsha
 kwa maafisa wa mipakani kuhusu usimamizi wa mazao na bidhaa zitokanazo 
na Bioteknolojia ya kisasa. Kulia ni Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya 
Makamu wa Rais Mazingira Dkt. Julius Ningu na kushoto ni Afisa Mazingira
 Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi Esta Makwaia. Warsha hii imefanyika leo
 kwenye Hotel ya La kairo jijini Mwanza
Washiriki
 wa Warsha ya Usimamizi wa mazao na bidhaa zitokanazo na bioteknolojia 
ya kisasa wakiwa kwenye picha ya pamoja na mgeni rasmi (katikati) Mara 
baada ya kufungua warsha hiyo kwenye Hoteli ya La kairo Jiji Mwanza
 …………………………………………….
Lulu Mussa na Ali Meja
Mwanza
 Imeelezwa kuwa Tanzania kama nchi
 nyingine haiwezi kukwepa maendeleo ya bioteknolojia kutokana na 
utandawazi na maendeleo duniani kote, kwa kuwa bioteknolojia ya kisasa 
ni nyenzo muhimu katika kukuza uchumi na kupunguza umaskini, kuboresha 
kilimo, uzalishaji viwandani, afya na hifadhi ya mazingira.
 Hayo yamesemwa leo na Naibu 
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Eng. Ngosi Mwihava katika warsha ya
 siku moja kwa maafisa wa mipakani kutoka mikoa ya kanda ya ziwa, warsha
 iliyolenga kukuza uelewa kwa watendaji wanaosimamia mazao na bidhaa 
zitokanazo na bioteknolojia ya kisasa.
 Amesema, Serikali kwa kutambua 
mchango mkubwa unaoweza kupatikana kutokana na matumizi ya bioteknolojia
 ya kisasa katika sekta za afya, kilimo, viwanda na mazingira, imeridhia
 Itifaki ya Cartagena ya Mkataba wa Bioanuai mwaka 2003 kwa lengo la 
kuhifadhi mazingira kwa kuzingatia usalama katika usafirishaji,  kuunda 
na kupitisha mfumo wa kitaifa wa usimamizi wa matumizi salama ya 
Bioteknolojia mwaka 2007.
 Eng. Mwihava amewaasa watendaji 
katika maeneo ya mipakani kuwa na usimamizi madhubuti katika maeneo yao 
ya kazi kwa kuwa mipaka kati ya Tanzania na nchi nyingine ndiyo njia kuu
 za uingizaji wa mazao na bidhaa zitokazo nje.
 Pamoja na faida za bioteknolojia 
hiyo ya kisasa Eng. Mwihava amewataka watendaji hao kuwa makini na 
athari zinazoweza kutokana na matumizi ya teknolojia hiyo pale 
itakapotumiwa bila kufuata taratibu za usalama zilizowekwa.
 Warsha hii ya siku moja kwa 
imewashirikisha maafisa forodha, Maafisa Afya na watafiti wa Mazao 
kutoka Mikoa ya Mwanza, Mara na Kagera, kutoka Idara , wakala za 
Serikali na sekta binafsi.


No comments:
Post a Comment