Mgombea
 nafasi ya Uenyekiti wa UVCCM kata ya Kawe Amani Nkurlu (kulia) 
akirudisha fomu ya kugombea nafasi hiyo kwa Katibu wa UVCCM kata ya Kawe
 Bi. Aisha Katundu. 
Katibu
 wa UVCCM kata ya Kawe Bi. Aisha Katundu (kushoto) akipokea fomu 
aliyoijaza Bw. Amani Nkurlu kwa nafasi ya kugombea Uenyekiti UVCCM kata 
ya Kawe alipofika ofisini hapo leo saa 7 mchana.
Mgombea
 wa Uenyikiti wa UVCCM kata ya Kawe, Amani Nkurlu, akizungumza machache 
na Katibu wa CCM Kawe Bi. Aisha Katundu katika ofisi za CCM Kawe.
Amani Nkurlu akijaza fomu ya kugombea nafasi ya Uenyekiti wa UVCCM kata ya Kawe.
Baadhi
 ya wakereketwa wa CCM katika picha ya pamoja nje ya ofisi ya CCM Kawe. 
Kutoka kushoto ni Katibu Mwenezi wa tawi la Umbwelani Kawe- Ramadhani 
Malenge, Katibu wa Wazazi Kawe- mama Katenda, mgombea nafasi ya ukatibu 
UVCCM kata ya Kawe – Sambili Tegemeo na mgombea nafasi ya Uenyekiti 
UVCCM kata ya Kawe – Amani Nkurlu.Picha na Josephat Lukaza
Baada
 ya uchaguzi wa UVCCM katika kata la Kawe kuvurugika mapema mwaka huu, 
uchaguzi huo unaorudiwa sasa umefika patamu ikibakia siku moja tu 
kuchukua fomu huku vijana wengi wakijitokeza kuwania nafasi mbali mbali 
katika jumuiya hiyo ya vijana illiyopo wilayani Kinondoni. 
Akizungumza
 na waandishi wa habari, mmoja wa wagombea wa Uenyekiti wa UVCCM katika 
kata hiyo, Amani Nkurlu (23) alisema “Siku zote nimekuwa nikitafakari ni
 kwa namna gani nitaweza kutoa mchango wangu katika chama na kuchangia 
mustakabali wa taifa letu Tanzania kwa ujumla.”
“Ninaamini
 CCM bado inahitaji vijana makini na wengi zaidi wakukisemea, kuishauri 
na kuleta chachu ya maendeleo katika utendaji wake wa kazi wa kila siku 
kichama na kiserikali. Hii ndio dira yangu kwa CCM, nina imani na chama 
changu na nimejikita katika kuchangia mabadiliko hayo kupitia Umoja wa 
Vjiana,” Nkurlu alisema. 
Nkurlu
 ambaye ana Shahada ya Mawasiliano kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu 
Agustino (SAUT) ameshawahi kushika nyadhifa mbali mbali za uongozi 
ukiwemo; Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM – Tawi maalum la Kambarage SAUT, 
Waziri wa Mambo ya Nje, Mbunge katika serikali ya wanafunzi, na Rais wa 
AIESEC akiwa hapo hapo chuoni. Mwaka 2010 Nkurlu pia alipata kugombea 
nafasi ya Umakamu wa Rais katika serikali ya wanafunzi chuoni hapo 
lakini hakufanikiwa kwa kupata kura 1278 kati ya kura 2995 zilizopigwa 
na 54 kuharibika.
Hivi
 sasa Nkurlu anamalizia Stashahada ya juu kutoka Chuo cha Diplomasia na 
pia ni mwajiriwa katika moja ya makampuni ya mawasiliano na matangazo 
jijini Dar es Salaam kama Mshauri wa Mawasiliano.
No comments:
Post a Comment