TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, December 26, 2012

PELEKENI WATOTO KWENYE CHANJO – WAZIRI MKUU

 
*Ahimiza matumizi ya vyandarua kujikinga na malaria
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amewataka Watanzania wote kushiriki chanjo ya kuzuia kichomi na kuhara kwa watoto pindi itakapoanza kutolewa mapema mwakani. 
Ametoa wito huo wakati akizungumza na maelfu ya wakazi wa kata ya Kibaoni na kata jirani za Ikuba, Usevya, Mbede, Mamba na Majimoto walioshiriki kula naye chakula cha mchana kuadhimisha sikukuu ya Krismasi.
Sherehe hizo zilifanyika kwenye uwanja wa shule ya msingi Kakuni ambako pia ni kijijini kwake kata ya Kibaoni, wilayani Mlele, mkoani Katavi.
“Serikali itaanza kutoa chanjo ya kuzuia kichomi (kitaalam wanaiita pneumonia) na ya kuzuia kuhara. Magonjwa haya mawili yana madhara makubwa kwa watoto wadogo. Natoa wito kwa Watanzania wake kwa waume, wakati ukifika wapelekeni watoto kwenye hiyo chanjo ili kuokoa maisha yao,” alisisitiza.
Alitumia fursa hiyo kuwahimiza wakazi wa kata hizo kununua vyandarua na kuvitumia ili kujikinga na ugonjwa wa malaria kwa vile ndiyo unaoongoza kwa vifo nchini kuliko magonjwa mengine.
“Nawasihi wafugaji, ninyi mna hela… uzeni mifugo ili mpate fedha ya kununua chandarua, takwimu zinaonyesha kuwa kila baada ya dakika tano kuna mgonjwa anakufa kutokana na malaria. Kwa hiyo mtu akipata visenti vyake, anunue chandarua kwa mkewe na watoto,” alisisitiza.
Akizungumzia kuhusu UKIMWI, Waziri Mkuu alitaka wakazi wa jimbo lake la Katavi kutambua kwamba ugonjwa huo upo na kwamba hauna tiba na tena hauchagui kijana wala mzee, kijana wa kiume au wa kike.

No comments:

Post a Comment