TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, December 27, 2012

MWANDISHI MOBINI SARYA NA SAFARI YAKE YA VISIWA VYA NYAMANGO NA CHEMBAYA MKOANI MWANZA

Mkurgenzi wa Tanpress Mobini Sarya akiwa kwenye usafiri wa pikipiki akitoka kwenye visiwa vya Nyamango na Chembaya eneo la Mwalo wa Kanyara ziwa Victoria mkoani Mwanza ambako alikwenda kuchunguza upatikanaji wa  huduma za afya katika visiwa hivyo  Novemba mwaka huu.
 
Hii ndiyo ofisi ya kijiji cha Lushamba inayohudumia visiwa saba vyenye wakazi elfu 25 .
 
Hii ndiyo ofisi ya kitongoji cha Kanyara kwa juu kama inavyoonekana kwa chini ni Sero (Mahabusu)inayotumika kuwahifadhi wa halifu ambayo mwandishi wa habari  Mobini Sarya aliwekwa chini ya ulinzi kwa masaa 6.
Wakazi wa kisiwa cha  Nyamango na Soswa wakigombania usafiri wa boti kwa ajili ya kuelekea Sengerema mkoani Mwanza.
……………………………………………………………
Nyamango/Soswa visiwa vyenye fursa tele za uwekezaji
zinahitajika zahanati,shule na kumbi za starehe.
Na Tanpress,Nyamango
NYAMANGO na Chembaya ni visiwa viliopo maili 46 Mgharibi mwa jijini Mwanza ingawa vinahesabiwa kuwa vipo wilayani Sengerema  Mkoa wa Mwanza.
Hivi visiwa vina undwa na vitongoji viwili vyenye visiwa vinne vikijulikana kwa majina ya kitongoji cha Nyamango/Chamagati na Chembaya/soswa vikiwa maeneo ya karibu. 
Vinakisiwa kuwa na wakazi zaidi ya 10,000 ambao wanategemea shughuli za uvuvi wa dagaa na samaki wanaopatikana katika ziwa viktoria.
Usafiri unaotumika kwenda kwenye visiwa hivyo ni boti au meli za watu binafsi,ambazo hutumia  masaa 12 kutoka jijini mwanza eneo hilo na mara nyingi boti ya mwendo kasi huingia saa mbili usiku.
Aidha kutoka katika visiwa hivi hadi kwenye mwalo wa Kanyara ambayo ni nchi kavu ya wilaya ya Sengerema boti hutumia masaa manne hadi masaa matatu kufika nchi kavu.
Pia kutoka eneo la kitongoji cha Kanyara usafiri ni wa shida Km.80 hadi kufika Sengerema mjini zilipo huduma zote za kijamii.  
Eneo hilo lina vitongoji viwili vinavyoundwa na visiwa vine ambavyo ni Soswa/Chembaya na Nyamango/Chamagati ni katika eneo hilo lenye makazi ya kudumu ya watu ndipo frusa za uwekezaji zipojitokeza.
Hivi karibuni Mwandishi wa Shirika la habari Tanpress alifika kwenye visiwa hivyo kwa lengo la kukusanya habari na matukio ndipo alipojionea frusa nyingi za uwekezaji.
Kwanza licha ya kwamba wavuvi wengi ni watu wanaopenda starehe hasa za ulevi lakini ‘viwanja vyakujirusha’kuburudika ni kama havitoshi.
Maeneo mbalimbali ambayo mwandishi wa Tanpress alitembelea alikuta wenyeji wakipata vinywaji kwenye baa zinazofanana na vilabu vya Pombe za kienyeji jambo linaloonyesha kuwa maeneo hayo yanahitajika uwekezaji wa baa na mahoteli ya kisasa.
Aidha nishati ya umeme kwenye eneo hilo inahitajika kwa haraka kwani wengi wanatumia jeneretor ambazo hawamudu kununua mafuta hivyo hata wale wachache waliojitolea kujenga nyumba za kulala wageni wanawasha vibatari wasijue la kufanya.
Hivyo anahitajika ,mwekezaji mkubwa aweke mashine inayotumia mafuta ya diseli kwa ajili ya kuzalisha umeme wa kutosha katika eneo hilo,ambalo kwasasa lipo gizani ingawa wenyeji wanahitaji huduma hiyo.
Pia sio lazima itumike mashine ya mafuta pia hata umeme wa jua au kufuka mitambo ya upepo kwasababu maeneo yale hakuna miti ya kuzuia upepo huo.
Baadhi ya maeneo ,mengine au hata visiwa vingine  mashine za kufua umeme kwa kutumia mafuta ya diseli ndio zinatumika kusambaza umeme jambo ambalo halijafanyika kwenye visiwa vya Nyamango.
Frusa nyingine uwekeza ambayo inalipa  ni kituo cha afya au zahanati,licha ya kwamba wavuvi wanafamilia zinazohitaji huduma ya afya wanapo ugua au akinamama wanapotaka kujifungua huduma hiyo haipo kabisa kwenye visiwa hivyo.
Kwa hiyo akitokea mwekezaji akafungua zahanati yenye uwezo wa kuzalisha akinamama wajawazito anaweza akanufaika kwa haraka kwasababu inavyoonekana serikali imeamua kutelekeza wakazi hao na haina mpango wowote wa kuwajengea zahanati.
Kwasasa zahanati sio jambo la mjadala inahitajika kwa haraka kuweza kuokoa maisha ya akinamama wajawazito na watu wa kawaida wanao umia kwenye starehe zikiwemo ulevi.
Ni vyema kama mwekezaji anavutiwa na uwekezaji huo akajenga kabisa kituo kikubwa cha afya kwasababu hakuna kituo karibu hata kwenye visiwa vya jirani kama zilagula na Yozwa bado huduma hiyo wana kwenda kuitafuta mbali.
Elimu ni frusa nyingine ya uwekezaji inayohitaji watu wenye mitaji kwani pamoja na kwamba wavuvi hao wanafamilia zao eneo hilo lakini kuna shule moja ya umma ambayo hata hivyo haitoshi mahitaji.
Shule hiyo ya msingi inajulikana kama Soswa shule ya Msingi bado haijaweza kutoa elimu bora kutokana na kukosekana kwa walimu wa kutosha eneo la visiwa hivyo.
Kwa hiyo zinahitajika shule za awali kwa kila kisiwa ambapo  kuna visiwa vinne pia zinatakiwa  shule binafsi za sekondari na msingi au hata vyuo vya michezo ya majini kwa ajili ya wagoeleaji.
Frusa zingine niliziona ni kuweka boti za mwendo kasi kwa ajili ya kuwakimbiza wagonjwa hospitalini na kuanzisha kampuni za ulinzi kwani hivi sasa baada ya uvamizi kuwepo, wakazi wa pale wameanza kukodi walinzi kutoka Mwanza ambapo ni mbali zaidi.
Zipo frusa nyingi za uwekezaji hata kwenye soko la chakula cha kuku na wanyama wengine lakini kama wewe ni mwekezaji unaweza kufika huko ukajionea mwenyewe.
www.mobinday.blogsopot.com 0753399 579 mobinsons@yahoo.com

No comments:

Post a Comment