Mkaguzi
 Msaidizi wa Polisi ambaye ni Polisi Tarafa wa Muklati Elibariki Kileo 
akitoa taarifa kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi 
Mwandamizi wa Polisi (SACP) Liberatus Sabas wakati wa makabidhiano ya 
kikosi kazi cha askari 15 watakaofanya kazi pamoja na wananchi wa Tarafa
 ya Muklati wilayani Arumeru. (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la 
Polisi Arusha) 

Kamanda
 wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) 
Liberatus Sabas akitoa elimu ya Polisi Jamii kwa viongozi, vikundi vya 
ulinzi shirikishi na wananchi wa Tarafa za Muklati na Enaboishu wilayani
 Arumeru. Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha)
Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha
Askari wa Jeshi
 la Polisi pamoja na viongozi wa Tarafa za Muklati, Enaboishu, Poli, 
Mbuguni  Moshono na King’ori zilizopo katika wilaya ya Arumeru 
wametakiwa kuungana na kufanya kazi kwa pamoja ili kuweza kufanikisha 
dhana nzima ya Ulinzi Shirikishi. 
Akiongea
 katika vikao tofauti vilivyofanyika mwishoni mwa wiki hii wakati wa 
kusambaza askari 15 kwa kila Tarafa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha 
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Liberatus Sabas alisema 
ushirikiano huo utafanikiwa endapo tu askari Polisi watakuwa wanatumia 
lugha nzuri na kufanya kazi kwa maadili huku viongozi wa Tarafa, Kata, 
Mitaa au vijiji watakuwa tayari kuwapa ushirikiano.
“Kama
 kutakuwa na ushirikiano wa dhati ambao utawezesha kufanya kazi kama 
timu moja basi kutakuwa na kuelezana ukweli na hivyo kuondoa majungu 
badala ya kila kundi kufanya kazi kwa kujitenga”. Alisema Kamanda Sabas.
Kamanda
 Sabas alisema serikali wanayoitumikia ni moja hivyo ili kukidhi malengo
 ya kuimarisha Ulinzi na Usalama katika maeneo yao makundi hayo 
yanatakiwa kuungana na kufanya kazi kama familia moja hali ambayo 
itasaidia kuongeza vikundi vya ulinzi shirikishi, kupata taarifa za 
uhalifu na wahalifu na hatimaye kupunguza vitendo vya uhalifu kama si 
kuutokomeza kabisa.
Alisema
 siku zote wahalifu wanafanikiwa sehemu ambazo ni dhaifu na zile sehemu 
ambazo zimeungana wanashindwa kupenya kwani uhalifu wowote ambao 
unahusisha watu wa mbali unaanzia toka kwa mwenyeji hivyo kama kila 
mwenyeji ataungana na wenzake kwa kuukataa uhalifu basi daima maeneo yao
 yatakuwa salama.
Kamishna
 huyo Msaidizi Mwandamizi wa Polisi pia aliwaomba wananchi hao 
kujitokeza mahakamani pindi wanapotakiwa kutoa ushahidi hali ambayo 
itasaidia kuwatia hatiani watuhumiwa watakaowakamata kinyume cha hapo 
jamii itaendelea kuvivyooshea vidole jeshi la Polisi pamoja na Mahakama.
Kwa
 upande wake Diwani wa Kata ya Ngaramtoni iliyopo katika Tarafa ya 
Muklati Bw. David Kimisi (CCM) alimpongeza Kamanda Sabas kwa hatua yake 
ya kuamua kutembelea Tarafa zote za Mkoa huu kwa nia ya kutoa elimu ya 
Polisi Jamii kwa viongozi, vikundi vya Ulinzi Shirikishi pamoja na 
wananchi na pia hatua yake ya kusambaza askari hao 15 kila tarafa ili 
waweze kutoa huduma karibu na jamii.
Diwani
 huyo alisema katika Tarafa yake kuna ushirikiano mkubwa kati ya 
Viongozi, wananchi ambao wanashirikiana vema na Mkaguzi wa Polisi wa 
Tarafa hiyo Elibariki Kileo pamoja na askari wa Tarafa hiyo hali ambayo 
imesaidia kwa kiasi kikubwa kupungua kwa vitendo vya uhalifu na 
wahalifu.
Alimalizia
 kwa kusema maneno ya Kamanda Sabas yameongeza chachu ya kuimarisha 
ulinzi katika eneo hilo huku viongozi na wananchi wa eneo hilo wakiwa na
 mipango dhabiti ya kukikarabati kama si kujenga kituo cha Polisi 
 kingine ili kiweze kuhudumia idadi kubwa ya watu wa eneo hilo kwa 
wakati mmoja.

No comments:
Post a Comment