Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
 akisikiliza maelezo kutoka kwa Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Peter, 
Stephano Kaombe, kuhusu maendeleo ya ujenzi wa Ukumbi wa mikutano wa 
Kanisa la Mtakatifu Peter lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam, 
wakati wa harambee ya kuchangia ujnenzi wa Ukumbi huo iliyofanyika leo 
asubuhi Jan 26, 2014. Picha na OMR
Makamu
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
 akisalimiana na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, wakati 
alipowasili kwenye Kanisa la Mtakatifu Peter Oysterbay, leo asubuhi kwa 
ajili ya kushiriki katika Harambee ya kuchangia Ujenzi wa Ukumbi wa 
mikutano wa Kanisa hilo. ambapo zaidi ya Sh. milioni 65 zilipatikana 
kati ya Sh. milioni 600, zinazohitajika hadi ifikapo mwezi Julai. Kati 
ya hizo Cash ni Sh. milioni 5 na zilizobakia zikiwa ni ahadi.Picha na 
OMR 
Picha ya pamoja 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Bilal, 
akiongoza na na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, kutoka kanisani baada ya 
ibada hiyo. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib
 Bilal, akizungumza na waumini wa dini ya Kikristu wakati wa Ibada 
maalum ya Harambee ya kuchangia ujenzi wa Ukumbi wa mikutano wa Kanisa 
la Mtakatifu Peter lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam, leo asubuhi 
Jan 26, 2014. Picha na OMR 

Makamu
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
 akisalimiana na Mwadhama Cardinari Polycap Pengo, wakati wa ibada 
maalum ya Harambee ya kuchangia ujenzi wa Ukumbi wa mikutano wa Kanisa 
la Mtakatifu Peter lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam, leo asubuhi 
Jan 26, 2014. Picha na OMR 
Baadhi ya waumini wa dini ya Kikristu waliohudhuria Ibada hiyo kwenye ibada hiyo.
Makamu
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Bilal, akiongoza na na
 Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, kutoka kanisani baada ya ibada hiyo. 
Makamu
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
 akizungumza na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa wakati 
alipotembelea kukagua maendeleo ya ujenzi wa ukumbi wa mikutano wa 
Kanisa la Mtakatifu Peter, baada ya ibada maalum ya harambee ya 
kuchangia ujenzi huo, iliyofanyika leo asubuhi, Jan 26, 2014. Kushoto ni
 Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Peter, Stephano Kaombe. Picha na OMR 
……………………………………………………………………….
Zaidi ya shilingi milioni 65 zimekusanywa
 katika harambee iliyoongozwa na Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib 
Bilal kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa ukumbi wa mikutano wa Kanisa la 
Mtakatifu Peter lililoko jijini Dar es salaam.
Kati
 ya fedha hizo zilizokusanywa katika ibada maalum ya kuchangia ujenzi wa
 jengo la ukumbi huo ilyoongozwa na Mhadhama Kadinali Polycap Pengo 
kiasi cha shilingi milioni 60.5 zilikuwa ni ahadi na  shilingi milioni 5
 zikiwa ni fedha taslimu. 
Akizungumza
 katika hafla hiyo, Makamu wa Rais aliwahakikishia Watanzania kuwa 
serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za taasisi za kidini katika 
kudumisha amani na upendo ndani ya jamii bila ya kujali tofauti za aina 
yo yote ile.
Alisema
 kuwepo kwake katika hafla hiyo ni ishara ya uhusiano mkubwa uliokuwepo 
kati ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Taasisi mbali 
mbali za dini  nchini.
“Sisi
 Watanzania tumefika hapa kutokana na uongozi thabiti wa waasisi wa 
Taifa letu. Hivyo, tunataka nchi ya watu wanaomwogopa Mungu, watu 
wanaopendana, watu wanaovumiliana na watu wanaotakiana mema katika 
shughuli zao.” 
Kwa
 mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi, Bibi Rose Rupia kamati yake 
inahitaji shilingi milioni 600 zaidi kukamilisha hatua za mwisho za 
ujenzi wa jengo la ukumbi huo na kwamba tayari wameshatumia kiasi cha 
shilingi bilioni moja katika ujenzi huo.
Ibada hiyo maalum ilihudhuriwa pia na viongozi mbali mbali akiwemo Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa.








No comments:
Post a Comment