
 Ni mara ya
 kwanza Saro kuzungumza tukio hilo tangu aliporuhusiwa kutoka Taasisi ya
 Mifupa na Mishipa ya Fahamu, MOI ya Hospitali ya Taifa Muhimbili 
alikokuwa amelazwa.Hakika @Ufoo Saro aliokoka kuuliwa mwaka jana 
mwishoni@
Mtangazaji
 wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Ufoo Saro ambaye alijeruhiwa kwa 
kupigwa risasi na mzazi mwenzake, Anthery Mushi, amefanya ibada na 
kusema: “Namshukuru Mungu kwa kumponya.”
Katika ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa la Kilutheli Tanzania (KKKT)
 Usharika wa Kibamba, Jimbo la Magharibi, Ufoo huku akitokwa na machozi 
na wakati mwingine kushindwa kuzungumza alisema: “Ni miujiza tu ya Mungu
 yeye kunifanya mimi kuwa hai leo.”
Mtangazaji huyo ambaye alilazwa kwa zaidi ya wiki mbili, aliwashukuru watu wote waliomtia moyo, kumsaidia kipindi chote alichokuwa mgonjwa.
“Sina
 cha kuwalipa, ninawashukuru sana kwa wema wenu, pia kwa kuniombea. 
Mungu ni mkubwa na amenipigania, naendelea vizuri kwa sasa,” alisema na 
kuongeza:
“Mungu
 alinisimamia na nyinyi pia mliniombea, hakika sina budi kushukuru kwa 
kila jambo. Nitasoma zaburi ya 146 katika Biblia Takatifu ili kumshukuru
 Mungu kwa kunisaidia.”
Ufoo alisema kuwa ameamua kumshukuru Mungu kwa sababu siyo watu wote wanaopata matatizo kama yake wanapona.
Mchungaji aliyeongoza misa hiyo iliyoanza saa 1 asubuhi hadi saa 5 asubuhi,Joseph Maseghe alisema Mungu hakupanga Ufoo afariki dunia kwa kupigwa risasi.
“Mungu
 bado anakuhitaji, hakupanga ndiyo maana upo nasi leo. Hautakiwi kulia 
huu ni mwanzo wa maisha yako mengine, usilie unachotakiwa ni kumshukuru 
Mungu kwa kila jambo,” alisema
No comments:
Post a Comment