Mhandisi
 wa mradi wa kiwanda cha kuchakata gesi asili kilichopo katika eneo la 
Madimba kinachosimamiwa na Shirika la Maendeleo na Petroli Tanzania 
(TPDC) Sultan Pwaga akitoa maelekezo kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda wakati wa ziara yake ya kikazi ya 
kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi asili 
kutoka Mtwara hadi Dar es salaam. Kushoto ni Waziri wa Nishati na Madini
 Prof. Sospeter Muhongo. 
Waziri
 Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda akitembelea 
maeneo mbalimbali kinapojengwa kiwanda cha kuchakata gesi asili eneo la 
Madimba mkoani Mtwara wakati wa ziara yake mkoani Mtwara. Kushoto ni 
Mkuu wa Mkoa wa huo Kapteni mstaafu Joseph Simbakalia, kulia ni Mhandisi
 wa mradi wa kiwanda cha kuchakata gesi asili  Sultan Pwaga
Meneja
 Mkuu Ujenzi kiwanda cha Dangote Tanzania Bhupendra Sharma akimwonesha 
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda moja ya 
mashimo ambapo itafungwa mitambo ya kiwanda cha kutegeneza saruji eneo 
la Msijute mkoani Mtwara. 

Waziri
 Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda akikagua baadhi 
ya vifaa ambavyo tayari vimeshafika eneo la Msijute mkoani Mtwara 
kinapojengwa kiwanda cha saruji cha Dangote Tanzania. 

Baadhi
 ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya sekondari Mstafa J.Sabodo 
wakimsikiliza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo 
Pinda alipowatembelea shuleni humo kuwapa pole kwa msimba wa wanafunzi 
sita baada ya kugongwa na gari wati wa mchakamchaka karibu na eneo la 
shulke yao. 

Waziri
 Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda na Mke wake Mama 
Tunu Pinda wakimjulia hali moja ya wanafunzi wa shule ya sekondari 
Mstafa J.Sabodo Chistopher Ngalapa (miaka 16 kidato cha pili) aliyelazwa
 katika Hospitali ya mkoa wa Mtwara Lugora baada ya kupata ajili tarehe 
Januari 22, 2014. 
 (Picha zote na Eleuteri Mangi- MAELEZO Mtwara )



No comments:
Post a Comment