TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, January 26, 2014

Ziara ya Waziri Mkuu mkoa wa Mtwara.

IMG_0135 
Mhandisi wa mradi wa kiwanda cha kuchakata gesi asili kilichopo katika eneo la Madimba kinachosimamiwa na Shirika la Maendeleo na Petroli Tanzania (TPDC) Sultan Pwaga akitoa maelekezo kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi asili kutoka Mtwara hadi Dar es salaam. Kushoto ni Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo. 
 IMG_2103 
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda akitembelea maeneo mbalimbali kinapojengwa kiwanda cha kuchakata gesi asili eneo la Madimba mkoani Mtwara wakati wa ziara yake mkoani Mtwara. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa huo Kapteni mstaafu Joseph Simbakalia, kulia ni Mhandisi wa mradi wa kiwanda cha kuchakata gesi asili  Sultan Pwaga
  IMG_2119 
Meneja Mkuu Ujenzi kiwanda cha Dangote Tanzania Bhupendra Sharma akimwonesha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda moja ya mashimo ambapo itafungwa mitambo ya kiwanda cha kutegeneza saruji eneo la Msijute mkoani Mtwara. IMG_2125
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda akikagua baadhi ya vifaa ambavyo tayari vimeshafika eneo la Msijute mkoani Mtwara kinapojengwa kiwanda cha saruji cha Dangote Tanzania. IMG_2143
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya sekondari Mstafa J.Sabodo wakimsikiliza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda alipowatembelea shuleni humo kuwapa pole kwa msimba wa wanafunzi sita baada ya kugongwa na gari wati wa mchakamchaka karibu na eneo la shulke yao. IMG_2157
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda na Mke wake Mama Tunu Pinda wakimjulia hali moja ya wanafunzi wa shule ya sekondari Mstafa J.Sabodo Chistopher Ngalapa (miaka 16 kidato cha pili) aliyelazwa katika Hospitali ya mkoa wa Mtwara Lugora baada ya kupata ajili tarehe Januari 22, 2014.
 (Picha zote na Eleuteri Mangi- MAELEZO Mtwara )

No comments:

Post a Comment