Waziri
 wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo (katikati) akieleza hatua 
iliyofikiwa katika ujennzi wa bomba la gasi linalojengwa kutoka Mtwara 
hadi Dar es salaam kwa Waziri Mkuu na msafara wake. Kushoto ni Balozi wa
 China nchini, Lu Younqing. 
 
 
Mke
 wa Waziri Mkuu mama Tunu Pinda akimsikiliza Waziri wa Nishati na Prof. 
Madini Sospeter Muhongo akizungumzia ujenzi wa bomba la gasi eneo la 
Bungu mkoa wa Pwani. 
 
 
Waziri Mkuu Mizengo Pinda na msafara wake wakiangalia eneo utakapochimbwa mtaro wa kupitishia bomba la gesi. 
 
 
Mafundi wakiendelea na kazi ya kuunganisha mabomba kabla ya kuyalaza na kuyafukia chini kwenye mitaro 
 
 
Mkuu
 wa mkoa wa Lindi akiwa na Waziri Mkuu mara baada ya kuwasili mkoani 
humo na kuendelea na ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa bomba la gesi Mkurugenzi
 Mtendaji wa kiwanda cha saruji cha MEIS Merea Barabuu akimkaribisha 
Waziri Mkuu Mizengo Pinda katika hafla ya uzinduzi wa kiwanda hicho 
kilichopo eneo la Machole Mkoani Lindi. 
 
 
Waziri
 Mkuu Mizengo Pinda akiwahutubia wananchi na wafanyakazi wa ujenzi 
kiwanda cha MEIS faida zitzkazotokana na kiwanda hicho ikiwa ni pamoja 
na upatikanaji wa gasi kijijini hapo kwa njia rahisi baada ya 
kuunganishwa kutoka bomba kuu la gasi ikiwemo ajira kwa wanachi na 
upatikanaji wa saruji kwa bei nafuu ili kuboresha makazi yao. 
 
 
Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa kiwanda cha MEIS kilichopo eneo la Machole Mkoani Lindi. 
 
 
Picha ya sura na muonekano wa kiwanda cha MEIS kitakapokamilioka
……………………………………………………………………………………..
Na Eleuteri Mangi-Maelezo Mtwara
SERIKALI
 imewapa jukumu wananchi wanaoishi maeneo linapopita  bomba la 
kusafirishia gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam la kulitunza na 
kulilinda  kwa manufaa yao na taifa zima.
Wito
 huo ulitolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo
 Pinda  leo alipokuwa katika ziara ya kikazi kukagua maendeleo ya ujenzi
 wa mradi wa bomba hilo.
Waziri
 Mkuu Pinda alisema Serikali inavihakikishia vijiji lilipopita bomba 
hilo kuwa watapatiwa umeme unaotokana na uzalishaji wa gasi na utakuwa 
wa gharama nafuu.
Zaidi
 ya hayo, gasi itatumika kwa matumizi ya nyumbani kwa kuunganishiwa 
bomba la gasi na ambao hawatafanikiwa watakuwa na fursa ya kupata 
mitungi ya gesi ambayo itakuwa ya bei nafuu.
Waziri
 Mkuu ameagiza mashirika ya Shirika la gasi na Petroli Tanzania (TPDC) 
na Mradi wa Nishati Vijijini (REA) wachukue jukumu la kuboresha maisha 
ya wananchi wa maeneo lilipopita bomba hilo katika maeneo ya barabara, 
shule, kuwapatia maji safi na salama,kuwaboreshea utoaji wa huduma za 
afya kwa kuboresha zahanati na vituo vya afya kama mchango wao kwa 
jamii.
Kwa
 upande wake Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo alisema 
kuwa serikali kupitia shirika la TPDC na REA itahakikisha wanachi 
waishio vjijini wanapata umeme mapema iwezekanavyo.
Kwa
 kuthibitisha kauli hiyo Prof. Muhongo alisema serikali kupitia TPDC na 
REA imetenga sh. Bilioni 20 kwa awamu ya kwanza ambayo itasimamiwa na 
REA wakati awamu ya pili nayo itatumia bilioni 20 iotkaysimamiwa na 
TPDC.
Katika
 ziara hiyo Waziri Mkuu aliambatana na mke wake bi Tunu Pinda, Balozi wa
 China nchini, Lu Younqing, Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospeter 
Muhongo, mbunge wa Mchinga Said Matanda na Fatma Mikidadi mbunge wa viti
 maalum. 
Maeneo aliyotembelea Waziri Mkuu ni pamoja na Vikindu, Jopika, Bungu, Ikwiriri, Somanga, Somanga Fungu, Kitomanga na Lindi.

No comments:
Post a Comment