Meneja
 Huduma wa Kliniki ambaye pia alimwakilisha Mganga Mkuu wa Hospitali ya 
Mkoa wa Morogoro, Abel Mtungi (kushoto), akimkabidhi Kamanada wa Polisi 
Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga, 
taarifa ya zoezi la upimaji afya kwa madereva wa mabasi ya abiria na 
malori iliyofanywa wakati wa Wiki ya Nenda kwa Usalama katika Kituo cha 
Mizani cha Mikese, mkoani Morogoro mwaka jana. Anayeshuhudia ni 
Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve
 Kilindo. TBL ilifadhili zoezi hilo.
 Mteknolojia
 Maabara wa Hospitali ya Tumbi, Kibaha, mkoani Pwani, Johannes 
Rwenyagila (kushoto) akimkabidhi Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama 
Barabarani Tanzania, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga, taarifa ya zoezi la
 upimaji afya kwa madereva wa mabasi ya abiria na malori lililofanywa 
wakati wa Wiki ya Nenda kwa Usalama katika Kituo cha Mizani cha Msata, 
mkoani Pwani mwaka jana. Anayeshuhudia ni Mkurugenzi wa Uhusiano na 
Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo.
 Afande
 Mpinga (wa pili kulia) akiwa na Kilindo wa TBL pamoja na madakari  
waliowasilisha utafiti huo. Meneja Huduma wa Kliniki ambaye pia 
alimwakilisha Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, Abel Mtungi 
 na Mteknolojia Maabara wa Hospitali ya Tumbi, Kibaha, mkoani Pwani, 
Johannes Rwenyagila
 Mkurugenzi
 wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo 
(wa pili kulia) akizungumza baada ya madaktari wa Hospitali za Tumbi na 
Morogoro (hawapo pichani), kukabidhi matokeo ya upimaji wa afya za 
madereva 800 mabasi ya abiria na malori wakati wa maadhimisho ya Wiki ya
 Usalama Barabarani, mwaka jana katika vituo vya mizani vya Mikese 
Morogoro na Msata Pwani. Zoezi hilo lilifadhiliwa na TBL. Aliyepokea 
taarifa ya matokeo hayo, Dar es Salaam juzi,  ni Kamanda wa Polisi 
Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga. 
Kutoka kushoto ni Ofisa Uhusiano wa TBL, Doris Malulu na Berther Mturi 
wa TBL.
Mteknolojia
 Maabara wa Hospitali ya Tumbi, Kibaha, mkoani Pwani, Johannes 
Rwenyagila  (katikati), akielezea jinsi walivyoendesha zoezi hilo. Kulia
 ni Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria. Steve Kilindo pamoja na Afande  
Kahatano wa kikosi cha usalama barabarani Makao Makuu.
 
 Meneja Huduma wa Kliniki ambaye pia alimwakilisha Mganga Mkuu wa 
Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, Abel Mtungi (kushoto), akielezea jinsi 
walivyofanya utafiti huo.
 Kamanda
 wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Naibu Kamishna, 
Mohamed Mpinga (katikati) akielezea kufurahishwa na matokeo ya utafiti 
huo. 
Kamanda
 wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Naibu Kamishna, 
Mohamed Mpinga (kulia), akionesha moja ya matokeo ya utafiti. 
No comments:
Post a Comment