TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, January 28, 2014

CAPTAIN SAM CHEKINGO AFARIKI DUNIA.

Marehemu Captain Sam Chekingo
Habari zimetufikia punde kwamba rubani wa ndege maarufu nchini Captain Sam Chekingo amefariki dunia Jumanne asubuhi nyumbani kwake Kinondoni jijini Dar es salaam. Kwa mujibu wa rafiki wa karibu wa marehemu Balozi Cisco Mtiro, misa ya kumuombea marehemu itaanza saa nne asubuhi kesho Jumatano 29 Jan 2014 nyumbani kwake, kabla ya mwili wake kupelekwa katika makaburi ya Kinondoni saa tisa alasiri.

Marehemu Kepteni Chekingo atakumbukwa kama mmoja wa marubani mahiri na wa muda mrefu wa ndege za serikali alikotumikia toka enzi za Rais wa awamu ya kwanza hayati Mwalimu Nyerere. Alistaafu kazi serikalini na kujiunga na Umoja wa Mataifa akifanyia kazi zake Congo Brazaville, kabla ya kurejea nyumbani na kujiunga na ATC alikofanyia kazi hadi mauti yalipomkuta.

Mola aiweke Roho ya marehemu mahali pema peponi

AMINA

No comments:

Post a Comment