TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, January 26, 2014

Ziara ya Waziri Mkuu Lindi na Mtwara

04
Bi  Asha Ismail mkazi wa Kitomanga mkoani Lindi akitwishwa ndoo ya maji na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mizengo Pinda baada ya kuzindua kisima cha maji kilichojengwa na kampuni ya CCP inayojenga bomba la mafuta kutoka Mtwara kwenda Dar es salaam. 05
Mhandisi Baltazari Mrosso akitoa maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa bomba la gesi linalotoka Mtwara mpaka Dar es salaam kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mizengo Pinda wakati anakagua maendeleo ya ujenzi wa bomba hilo.
01
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mizengo Pinda akizindua na kuweka jiwe la msingi la kiwanda cha saruji cha MEIS eneo la Machole mkoani. 02
Sehemu iliyoandaliwa kitakapojengwa kiwanda cha saruji cha MEIS eneo la Machole mkoani. 03
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mizengo Pinda akitembelea baadhi ya maeneo ya kiwanda cha saruji cha MEIS  baada ya kikizindua.

No comments:

Post a Comment