TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, January 28, 2014

DC Kiteto, Emboley Murtangos aaswa kutowabughudhi wakulima 50

Na:BERNAD DANIEL

Mwenye miwani ni Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Martha Umbula na Jane Mutagurwa Mkurugenzi wa Halamshauri ya Wilaya ya Kiteto
 
NA.MOHAMED HAMAD
 
Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara Martha Umbulla ameaswa kuacha kuwaondoa wakulima 50 waliofungua kesi dhidi ya Halamshauri katika eneo linalogombaniwa la Emboley Murtangos kuwa waachwe kwa kuwa kesi iko mahakamani
Kesi iko mahakama ya Rufaa yenye namba 140/2012, imepangwa kusikilizwa Feb 13 mwaka huu kwamba hivi karibuni Mkuu wa Wilaya alitoa amri kuwataka watu wote wanaoishi na kufanya shughuli za kibinadamu kilimo,ufugaji,na uchomaji mkaa watoke kuwa waachwe mpaka kesi imalizike
Jumla ya wakulima 50 wakiongozwa na Tito Shumu walifungua kesi ya msingi kupinga amri ya Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto kuvunja makazi yao kwa madai kuwa wamevamia na kuanzisha vitongoji haramu kwa kufanya shughuli za kilimo
Kwa mujibu wa barua ya Wakili G. S. OKWONG’A anaye watetea wakulima ya Jan 23 mwaka huu kwa Mkuu wa Wilaya ya Kiteto kupitia amri yake ya Jan 21 .2014 kuwataka wakulima hao kuondoka ameombwa kusitisha kutokana na kuwepo kesi inayoendelea mahakama ya Rufaa Dar
“Mheshimiwa kwa kuwa kuna kesi ya msingi Mahakama ya Rifaa na imepangwa kusikilizwa tarehe 13/2/2014 tunakuomba utumie busara zako kusitisha amri ya kuwaondoa wateja wetu katika eneo lenye mgogoro mpaka hapo kesi itakaposikilizwa na kutolewa maamuzi”ilisema sehemu ya barua hiyo
Hata hivyo pamoja na taarifa hiyo ya kimaandishi kwa Mkuu huyo wa Wilaya pia alipatiwa viambatanisho vya vivuli vya wito wa Mahakama na pia hoja ya maandishi aliyoitoa ya kuwataka watu wote waliopo katika eneo la Emboley Murtangos waondoke mara moja
“Watu wote wanaoishi na kufanya shughuli za kibinadamu, hususani kilimo,ufugaji,uchomaji wa mkaa katika eneo lote la Hifadhi ya Emboley Murtangos muondoke mara moja kulingana na amri iliyotolewa na Mahakama ya Rufaa Tanzania mwaka 2012”
“Kwa mujibu wa mamlaka niliyopewa mnatakiwa muondoke wote ndani ya siku mbili kuanzia  Jan 21-23 mwaka huu,yeyote atakayekaidi amri hii atachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa kosa la kutokutii amri halali ya mahakama”ilieleza amri hiyo ya Mkuu wa Wilaya
Amri hiyo imekuwa ikitolewa na baadhi ya viongozi mbalimbali wa Wilaya, Mkoa,na hata Taifa kuwa pamoja na kufahamu suala hili liko mahakamani, wamekuwa wakiwahadaa wananchi na kuwapa usumbufu uliodaiwa kuleta madhara makubwa kwao
Jan 16 mwaka huu Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliyewasili Wilayani Kiteto kutoa pole kutokana na maafa ya watu 10 yaliyofanywa na kikundi cha watu wachache kwa maslahi yao binafsi ambapo aliagiza wakamatwe mara moja na kufikishwa mahakamani
Jumla ya watu 35 walikamatwa na Polisi, 12 walifikishwa mahakamani na kufunguliwa kesi ya mauaji, 10 wako chini ya uangalizi wa Jeshi la Polisi,7 waliachiwa huru  baada ya Polisi kujiridhisha na wengine 6 wanaendelea kuhojiwa juu ya mauaji ya watu 10 Jan 12 mwaka huu katika vitongoji vya Kwa Mtanzania na Laitime Wilayani humo.
Mwisho

No comments:

Post a Comment