TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, January 28, 2014

Cech ampeleka Diego Costa Chelsea

Ni kama golikipa Petr Cech wa Chelsea amempeleka mshambuliaji wa Atletico Madrid Chelsea baada ya golikipa wa Chelsea anayecheza kwa mkopo Atletico Madrid Thibaut Courtois kuhofia bench akiorudi kwenye timu hiyo na sasa anatumika kama chambo.

Chelsea na Atletico Madrid zinaelezwa kuwa zimefikia makubaliano ya kubadilishana wachezaji hao deal itakayomfanya Diego Costa kutua Stamford Bridge msimu ujao na Courtois kubakia Atletico,hii ni kwa mujibu wa media za Hispania.

Costa ametumbukia wavuni mara 19 msimu huu katika La Liga na hesabu kubwa za kocha wa Chelsea Jose Mourinho ni kunasa mshambuliaji.
Chelsea walimtaka Courtois kusaini mkataba mpya licha ya kwamba hajawahi kucheza kwenye timu hiyo lakini kipa huyo ameomba asajiliwe moja kwa moja Atletico

Awali Courtois alisema atarudi Chelsea endapo atakwenda kuwa golikipa chaguo la kwanza mbele ya Petr Cech kwasababu hawezi kwenda kwenye timu ambayo atasugua benchi,kwake kubwa ni kucheza iwe Chelsea au klabu nyingine.

No comments:

Post a Comment