MAHAKAMA
 ya mwanzo Mjini Namanyere, Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa imetoa amri ya 
kumtaka Ndebile Kazuri kujenga nyumba ya aliyekuwa mke wake Maria Tarafa
 iliyopo kijijini Isale ambayo aliibomoa akishinikiza mtalaka wake aondoke eneo ambalo alikuwa akikaa kabla ya kutengana.
Mwishoni
 mwa mwaka jana (2013) Mahakama hiyo ilivunja ndoa ya wanandoa hao wenye
 watoto wanne baada ya Kazuri kuwasilisha kesi mahakamani akitaka ndoa 
yake na mkewe ivunjwe. Hata hivyo baada ya kuvunjwa kwa ndoa hiyo mke 
amewasilisha kesi mahakamani hapo akitaka mali za ndoa hiyo zigawanywe 
na mume awajibike kuwatunza watoto wake, jambo ambalo halikuzungumziwa 
kwenye kesi ya awali.
Akizungumza
 na mwandishi wa habari hizi juzi, Bi. Tarafa alisema Mahakama ya mwazo 
imetoa amri ya kumtaka mtalaka wake kujenga nyumba aliyomvunjia yeye na 
watoto wake wanne akishinikiza aondoke nyumbani hapo, bila kupewa haki 
ya mgao wa mali zilizochumwa wakati wa ndoa.
“…Juzi
 tumetoka Mahakamani nilikwenda kufungua kesi nikiiomba mahakama igawe 
mali ambazo tulichuma na mume wangu muda wote wa ndoa yetu lakini mume 
wangu hataki zigawanywe, ila mahakama imemuamuru kwanza ajenge nyumba 
ambayo amenivunjia pale nyumbani nikiwa na watoto akitaka niondoke 
nyumbani, ameambiwa awe ameimaliza kabla ya Februari 14,” alisema Bi. 
Tarafa akizungumza kwa njia ya simu.
No comments:
Post a Comment