TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, December 3, 2013

BERKO RASMI MSIMBAZI, DHAIRA `BAI BAI`, VITA NA KASEJA WA YANGA KUENDELEA KAMA KAWAIDA!!

Na Baraka Mpenja , Dar es salaam
 
HATIMAYE `Deal Done`!!. Wekundu wa Msimbazi Simba Sc, Taifa Kubwa wamehalalisha kuondoka kwa kipa wake Mganda, Abel Dhaira baada ya leo hii kumsajili mlinda mlango wa zamani wa Dar Young Africans, raia wa Ghana, Yaw Berko kwa mkataba wa miezi 6.
Berko ametua leo jijini Dar es salaam  na pipa akitokea kwao Ghana, (Magharibi mwa Afrika) na amekuja kufanya kazi na kocha mpya wa klabu ya Simba,  Mserbia Zdravko Lugarusic ambaye pia  mchana wa leo amesaini mkataba wa miaka miwili kurithi mikoba ya kocha, Abdallah Athuman Seif `King Kibadeni Mputa` aliyabebeshwa virago kwa madai ya kushindwa kufanya vizuri mzunguko wa kwanza wa ligi kuu soka Tanzania bara.
Kusajili wa kwa Berko kumekalimisha safari ya Dhaira kufanya kazi Msimbazi kwani tayari uongozi wa klabu hiyo ulishaondoa imani juu ya kipa huyo wakidai kiwango chake hakiridhishi,  kwani amekuwa akifungwa mabao mepesi sana.
Vita kama kawa:  Berko kamwaga wino leo Msimbazi, mpinzani wake wa wakati ule akiwa Yanga, Juma Kaseja amejiunga na wanajangwani dirisha dogo la usajili, kutokana na ubora wa makipa hawa wawili, upinzani mkali unategemewa
Kipa huyo aliwadakia watani wa jadi wa Simba, Dar Young Africans tangu mwaka 2010 baada ya kujiunga katika dirisha dogo mnamo desemba mwaka 2009 akitokea kufanya kazi na klabu ya Ghana ya Liberty Proffessionals .
Berko alifanya kazi na Yanga  hadi msimu uliopita alipotolewa kwa mkopo kwenda kufanya kazi yake katika klabu ya FC Lupopo ya DRC Kongo.
Baada ya kufika mjini Lubumbashi, Berko alizingua kufanya kazi na kuamua kurejea jijini Dar es salaam kujiunga na Yanga kwa madai ya kutoridhishwa na hali ya klabu hiyo , lakini uongozi ulimtupilia mbali kwa kuuvunja mkataba wake na kumlipa `Mtonyo` wake  kwani tayari wakati huo walikuwa wameshapata kipya mpya Ally Mustapha ` Bartez` aliyetokea Simba na Berko akapaa angani kurejea kwao Ghana.
Kaseja Juma 
Tanzania One: Mlinda Mlango mpya wa Yanga, Juma Kaseja ataendelea kupambana na kipa mwenzake bora, Yaw Berko wa Simba.
Wakati Berko akiidakia Yanga, mpinzani wake langoni alikuwa kipa wa zamani wa Wekundu wa Msimbazi Simba sc, Juma Kaseja ambaye aliachwa na Simba msimu uliopita, lakini upinzani unaendelea tena baada ya Kaseja `Tanzania One` kujiunga na Yanga na leo hii ameanza mazoezi katika uwanja wa Bora kijitonyama, jijini Dar es salaam.
Kusajiliwa kwa Kaseja Yanga, kumemkutanisha tena na makipa wenzake wawili aliowahi kuwakalisha benchi kwa muda wote wakiwa Simba, Ally Mustapha `Bartez` na Deogratius Munish `Dida`.
Tusubiri maamuzi ya benchi la ufundi la Yanga chini ya kocha Mholanzi, Ernie Brandts kuamua ni kipa gani atakuwa chagua lake.
Leo hii katika mazoezi ya Yanga, makipa hao Bartez na Kaseja walikuwa kivutio walipokuwa wakifanya mazoezi pamoja chini ya kocha wa Makipa, Mkenya Razack Ssiwa

No comments:

Post a Comment