TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, December 2, 2013

VIJANA WA MWANYANAYA WASHIRIKI USAFI WA MAENEO ZANZIBAR

tamasha-vijana1 
Na Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi –Zanzibar
ZANZIBAR JUMATATU DESEMBA 2, 2013. Wananchi wa Shehia ya Mwanyanya nje kigogo ya mji wa Zanzibar wakiongozwa na Kikundi cha Vijana wa Green Society cha eneo hilo, wameshiriki katika kazi ya ukusanyaji na uzoaji wa taka katika shehia hiyo.
Wakizungumza mara baada ya kazi hiyo, Mwenyekiti wa Green Society Bw. Ali Abdallah Ali na Ali Bakari Khatibu, wamesema mbali ya kikundi hicho kushiriki katika kazi hiyo ya uzoaji taka, pia kikundi hicho kitaendelea na kazi ya ustawishaji wa mazingira ikiwa ni pamoja na kupanda miti ya kisasa na kuitunza ile ya uwoto wa aslai iliyopo katika eneo hilo.
Wamesema Kikundi hicho cha Mwanyanya Green Society kitahakikisha kuwa kila kijana na mwananchi wa eneo hilo la Mwanyanaya anashiriki kwa hali na mali katika kazi za usafi wa mazingira na kulifanya eneo la Mwanyanaya kuwa lenye kijani kibichi na lisilokuwa na taka.
Awali Mkuu wa Kitengo cha Elimu ya Mazingira Zanzibar Bi. Zuwema Juma Hamadi, ambaye alikuwa mgeni Rasmi katika shughuli hiyo, alisema kuwa ofisa yake imeanzisha operesheni ya uzuiaji wa uchimbaji wa mchanga kiholela ikiwa ni sehemu ya kuzuia uharibifu wa mazingira.
Vijana hao wa Green Society, wameitumia siku hiyo kama sehemu ya uzinduzi wa kikundi chao ambacho mbali ya kujihusisha na masuala ya ustawishaji wa mazingira pia kinalenga katika kumkwamua kijana katika matumizi ya dawa za kulevya na kumjengea mazingira ya kujiajiri.
Aidha Vijana hao wametoa wito kwa wananchi katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kujitolea katika masuala ya usafi na usawishaji wa mazingira kwani kwa kufanya hivyo kutaiwezesha nchi yetu kuwa ya kijani kibichi.

No comments:

Post a Comment