Na Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi –Zanzibar
ZANZIBAR
 JUMATATU DESEMBA 2, 2013. Wananchi wa Shehia ya Mwanyanya nje kigogo ya
 mji wa Zanzibar wakiongozwa na Kikundi cha Vijana wa Green Society cha 
eneo hilo, wameshiriki katika kazi ya ukusanyaji na uzoaji wa taka 
katika shehia hiyo.
Wakizungumza
 mara baada ya kazi hiyo, Mwenyekiti wa Green Society Bw. Ali Abdallah 
Ali na Ali Bakari Khatibu, wamesema mbali ya kikundi hicho kushiriki 
katika kazi hiyo ya uzoaji taka, pia kikundi hicho kitaendelea na kazi 
ya ustawishaji wa mazingira ikiwa ni pamoja na kupanda miti ya kisasa na
 kuitunza ile ya uwoto wa aslai iliyopo katika eneo hilo.
Wamesema
 Kikundi hicho cha Mwanyanya Green Society kitahakikisha kuwa kila 
kijana na mwananchi wa eneo hilo la Mwanyanaya anashiriki kwa hali na 
mali katika kazi za usafi wa mazingira na kulifanya eneo la Mwanyanaya 
kuwa lenye kijani kibichi na lisilokuwa na taka. 
Awali
 Mkuu wa Kitengo cha Elimu ya Mazingira Zanzibar Bi. Zuwema Juma Hamadi,
 ambaye alikuwa mgeni Rasmi katika shughuli hiyo, alisema kuwa ofisa 
yake imeanzisha operesheni ya uzuiaji wa uchimbaji wa mchanga kiholela 
ikiwa ni sehemu ya kuzuia uharibifu wa mazingira.
Vijana
 hao wa Green Society, wameitumia siku hiyo kama sehemu ya uzinduzi wa 
kikundi chao ambacho mbali ya kujihusisha na masuala ya ustawishaji wa 
mazingira pia kinalenga katika kumkwamua kijana katika matumizi ya dawa 
za kulevya na kumjengea mazingira ya kujiajiri.
Aidha
 Vijana hao wametoa wito kwa wananchi katika maeneo mbalimbali ya 
Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kujitolea katika masuala ya usafi na 
usawishaji wa mazingira kwani kwa kufanya hivyo kutaiwezesha nchi yetu 
kuwa ya kijani kibichi.

No comments:
Post a Comment