TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, December 5, 2013

Chadema yaijia juu Polisi tukio la moto Arusha,

lema+px
Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema.PICHA|MAKTABA 
……………………………………………………………………………………
Arusha.Polisi mkoani Arusha imekamilisha uchunguzi wake kuhusiana na kuungua kwa Ofisi za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kusema wanachama wa chama hicho ndio waliohusika.
Hata hivyo, Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amepinga kauli hiyo na kulipa jeshi hilo siku nne kuwakamata na kuwahoji watuhumiwa watano baada ya kulipatia majina hayo akidai kuwa ndio wanaohusika na uchomaji moto ofisi za chama hicho.
“Tumewapatia polisi majina… tunaamini walihusika moja kwa moja la sivyo, chama kitatumia vijana wetu wa Red Brigade kuwakamata na kuwafikisha polisi,” Lema aliwaambia waandishi wa habari jana.
Ofisi cha Chadema zilizoko katika eneo la Ngarenaro, zilinusurika kuteketea kwa moto juzi baada ya watu wasiojulikana kuwasha moto katika moja ya vyumba vyake.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Japhet Lusinga alisema:
“Katika uchunguzi wetu, tumebaini kuwa hakuna mahali palipovunjwa kutoka nje ya uzio na kuruhusu watu kuingia ndani… tumegundua kuna tundu dogo darini eneo la kuelekea bafuni la upana wa futi moja na nusu kiasi haliwezi kuruhusu mtu kupita.
“Tumejiridhisha kuwa hakuna mtu anayeweza kupita hapo na ndani tulikuta majivu na baadhi ya vitu vilivyoungua na vifaa vingine.”
Lema akiwa na Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Arusha, Ephata Nanyaro alisema: “Tumebaini polisi wanataka kulifanya jambo hili kama la siasa ndiyo sababu juzi badala ya kuanza kuchunguza waliohusika, waliwakamata Mtunza Ofisi na mlinzi wetu na kuwalaza rumande hadi leo (jana) asubuhi kwa madai eti wanawahoji.
“Hatukubaliani na taarifa yao, hii ni siasa. Kulitokea mauaji ya bomu, wakasema Chadema wamejilipua, leo ofisi imechomwa wanasema Chadema wenyewe, hili hatukubali, “ alisema.
Msajili alaani
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amelaani tukio la kuchomwa moto ofisi hizo za Chadema na kusisitiza kuwa wananchi hususan wanasiasa wasiwe wepesi kuingiza hisia kwenye makosa ya kijinai.
Alisema kuwa tukio hilo linapaswa kukemewa kwa hali yoyote ile kwa kuwa linavuruga na kuhatarisha amani ya nchi.
Dk Slaa aanza ziara
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa amesema hakuna mtu yeyote mkubwa kuliko katiba ya chama hicho.
Dk Slaa aliyasema hayo jana kwenye Uwanja wa CDT, Kahama mkoani Shinyanga, alipokuwa akihutubia mamia ya wanachama na mashabiki wa chama hicho akiwa katika ziara yake kuimarisha chama katika mikoa ya Shinyanga na Kigoma.
“Chadema ni chama makini, kina kila kitu kwenye katiba yake kuliko hata CCM, kina itifaki, kina maadili hata mimi na Mwenyekiti Mbowe (Freeman) imetuwekea mipaka ya utendaji… “Chama hakiwezi kumwonea mtu, kinatenda haki na yanayotokea sasa ni msukumo wa baadhi ya vyombo vya usalama na hayakuanza leo.”
Kauli yake ilionekana kutoa ufafanuzi wa hatua ya Kamati Kuu ambayo ilimvua nyadhifa zake zote aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe na wenzake wawili kwa madai ya kuandaa waraka kuhamasisha mabadiliko hatua iliyosababisha mvutano mkubwa ndani ya chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

No comments:

Post a Comment