
Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema.PICHA|MAKTABA  
……………………………………………………………………………………
Arusha.Polisi
 mkoani Arusha imekamilisha uchunguzi wake kuhusiana na kuungua kwa 
Ofisi za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kusema wanachama
 wa chama hicho ndio waliohusika.
Hata
 hivyo, Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amepinga kauli 
hiyo na kulipa jeshi hilo siku nne kuwakamata na kuwahoji watuhumiwa 
watano baada ya kulipatia majina hayo akidai kuwa ndio wanaohusika na 
uchomaji moto ofisi za chama hicho.
“Tumewapatia
 polisi majina… tunaamini walihusika moja kwa moja la sivyo, chama 
kitatumia vijana wetu wa Red Brigade kuwakamata na kuwafikisha polisi,” 
Lema aliwaambia waandishi wa habari jana.
Ofisi
 cha Chadema zilizoko katika eneo la Ngarenaro, zilinusurika kuteketea 
kwa moto juzi baada ya watu wasiojulikana kuwasha moto katika moja ya 
vyumba vyake.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Japhet Lusinga alisema:
“Katika
 uchunguzi wetu, tumebaini kuwa hakuna mahali palipovunjwa kutoka nje ya
 uzio na kuruhusu watu kuingia ndani… tumegundua kuna tundu dogo darini 
eneo la kuelekea bafuni la upana wa futi moja na nusu kiasi haliwezi 
kuruhusu mtu kupita.
“Tumejiridhisha kuwa hakuna mtu anayeweza kupita hapo na ndani tulikuta majivu na baadhi ya vitu vilivyoungua na vifaa vingine.”
Lema
 akiwa na Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Arusha, Ephata Nanyaro 
alisema: “Tumebaini polisi wanataka kulifanya jambo hili kama la siasa 
ndiyo sababu juzi badala ya kuanza kuchunguza waliohusika, waliwakamata 
Mtunza Ofisi na mlinzi wetu na kuwalaza rumande hadi leo (jana) asubuhi 
kwa madai eti wanawahoji.
“Hatukubaliani
 na taarifa yao, hii ni siasa. Kulitokea mauaji ya bomu, wakasema 
Chadema wamejilipua, leo ofisi imechomwa wanasema Chadema wenyewe, hili 
hatukubali, “ alisema.
Msajili alaani
Msajili
 wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amelaani tukio la 
kuchomwa moto ofisi hizo za Chadema na kusisitiza kuwa wananchi hususan 
wanasiasa wasiwe wepesi kuingiza hisia kwenye makosa ya kijinai.
Alisema kuwa tukio hilo linapaswa kukemewa kwa hali yoyote ile kwa kuwa linavuruga na kuhatarisha amani ya nchi.
Dk Slaa aanza ziara
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa amesema hakuna mtu yeyote mkubwa kuliko katiba ya chama hicho.
Dk
 Slaa aliyasema hayo jana kwenye Uwanja wa CDT, Kahama mkoani Shinyanga,
 alipokuwa akihutubia mamia ya wanachama na mashabiki wa chama hicho 
akiwa katika ziara yake kuimarisha chama katika mikoa ya Shinyanga na 
Kigoma.
“Chadema
 ni chama makini, kina kila kitu kwenye katiba yake kuliko hata CCM, 
kina itifaki, kina maadili hata mimi na Mwenyekiti Mbowe (Freeman) 
imetuwekea mipaka ya utendaji… “Chama hakiwezi kumwonea mtu, kinatenda 
haki na yanayotokea sasa ni msukumo wa baadhi ya vyombo vya usalama na 
hayakuanza leo.”
Kauli
 yake ilionekana kutoa ufafanuzi wa hatua ya Kamati Kuu ambayo ilimvua 
nyadhifa zake zote aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe na wenzake 
wawili kwa madai ya kuandaa waraka kuhamasisha mabadiliko hatua 
iliyosababisha mvutano mkubwa ndani ya chama hicho kikuu cha upinzani 
nchini.
No comments:
Post a Comment