TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, December 2, 2013

KAIJAGE: TANZANITE NI MAHINDI MACHANGA YANAYOCHIPUKIA, WASIKATISHWE TAMAA SAFARI YAO!!

DSC_0184
Na Baraka Mpenja - Dar es salaam
Wakati timu ya Taifa ya vijana ya wanawake chini ya miaka 20, maarufu kwa jina la Tanzanite ikijiandaa na Mechi ya kwanza ya raundi ya michuano ya Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika dhidi ya Afrika Kusini Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Desemba 7 mwaka huu, kocha mkuu wa timu za taifa za wanawake , Tanzanite na Twiga stars, Rogasian Kaijage amewaomba watanzania kuwatia moyo vijana hawa kwani hawajaanza kufanikiwa bado.
Kaijage amesema watanzania wasitegemee mafanikio ya haraka kwa timu hii na wale wasichukulie matokeo ya mwanzo kama mafanikio, bali wanatakiwa kuwapa moyo vijana hawa kwani safari yao ni ndefu mno.
“Watanzania tusiwae na tabia ya kutaka mafanikio ya haraka, hawa vijana bado wanayo safari ndefu, cha msingi watanzania hasa wapenda michezo wawape sapoti kubwa ili kufikia mafanikio”. Alisema Kaijage.
“Vijana hawa ni mahindi machanga ndio yanaanza kuchipua, kile wanachokifanya sio mavuno bali ni ishara kuwa wanatakiwa kuungwa mkono. Hawatakiwi kukatishwa tamaa, waungwe mkono kwani wanatengenezwa kwa ajili ya baadaye”. Aliongeza Kaijage.
Kocha huyo alisema katika soka lazima mipango iwekwe, watu wakubali kuwekeza, hivyo wapende michezo wajitokeza kudhamini timu za wanawake kwani wanao uwezo wa kufika mbali zaidi.
Akizungumzia mchezo ujao dhidi ya Afrika kusini, Kaijage alisema utakuwa mgumu sana kutokana na ubora wao, lakini kila kitu kinawezekana kutokana na maandalizi ya vijana wake.
“Vijana wanaendelea vizuri sana, ninaposema hivyo namaanisha wana morali ya kushindani ili kupata matokeo mazuri. Hivyo watanzania wajiandae kuwapa sapoti vijana wao”. Alisema Kaijage.
Tanzanite ilifuzu raundi ya pili baada ya kuifunga Msumbiji mabao 15-1 ambapo mechi ya kwanza jijini Dar es salaam waliwalamba 10-0 na mechi ya msumbiji wakaitungua 5-1.

No comments:

Post a Comment