Na Baraka Mpenja - Dar es salaam 
Wakati
 timu ya Taifa ya vijana ya wanawake chini ya miaka 20, maarufu kwa jina
 la Tanzanite ikijiandaa na Mechi ya kwanza ya raundi ya michuano ya 
Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika dhidi ya Afrika Kusini Uwanja wa Taifa, 
Dar es Salaam Desemba 7 mwaka huu, kocha mkuu wa timu za taifa za 
wanawake , Tanzanite na Twiga stars, Rogasian Kaijage amewaomba 
watanzania kuwatia moyo vijana hawa kwani hawajaanza kufanikiwa bado.
Kaijage
 amesema watanzania wasitegemee mafanikio ya haraka kwa timu hii na wale
 wasichukulie matokeo ya mwanzo kama mafanikio, bali wanatakiwa kuwapa 
moyo vijana hawa kwani safari yao ni ndefu mno.
“Watanzania
 tusiwae na tabia ya kutaka mafanikio ya haraka, hawa vijana bado wanayo
 safari ndefu, cha msingi watanzania hasa wapenda michezo wawape sapoti 
kubwa ili kufikia mafanikio”. Alisema Kaijage.
“Vijana
 hawa ni mahindi machanga ndio yanaanza kuchipua, kile wanachokifanya 
sio mavuno bali ni ishara kuwa wanatakiwa kuungwa mkono. Hawatakiwi 
kukatishwa tamaa, waungwe mkono kwani wanatengenezwa kwa ajili ya 
baadaye”. Aliongeza Kaijage.
Kocha
 huyo alisema katika soka lazima mipango iwekwe, watu wakubali kuwekeza,
 hivyo wapende michezo wajitokeza kudhamini timu za wanawake kwani wanao
 uwezo wa kufika mbali zaidi.
Akizungumzia
 mchezo ujao dhidi ya Afrika kusini, Kaijage alisema utakuwa mgumu sana 
kutokana na ubora wao, lakini kila kitu kinawezekana kutokana na 
maandalizi ya vijana wake.
“Vijana
 wanaendelea vizuri sana, ninaposema hivyo namaanisha wana morali ya 
kushindani ili kupata matokeo mazuri. Hivyo watanzania wajiandae kuwapa 
sapoti vijana wao”. Alisema Kaijage.
Tanzanite
 ilifuzu raundi ya pili baada ya kuifunga Msumbiji mabao 15-1 ambapo 
mechi ya kwanza jijini Dar es salaam waliwalamba 10-0 na mechi ya 
msumbiji wakaitungua 5-1.

No comments:
Post a Comment