Dar
 es Salaam: Mechi ya Nani Mtani Jembe kati ya Simba na Yanga 
zinazodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itachezwa Jumamosi, Desemba
 21, 2013 saa kumi kamili jioni kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es 
salaam. 
Akiongea
 na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo, Meneja wa Kilimanjaro 
Premium Lager, George Kavishe amesema “Tayari Simba na Yanga zimesaini 
makubaliano ya kucheza MECHI YA NANI MTANI JEMBE (NANI MTANI JEMBE 
MATCH). Pambano hili  ni zawadi ya kufungia mwaka kwa mashabiki na kila 
timu imetia sahihi makubaliano kwamba itachezesha kikosi cha kwanza ili 
kuwapa mashabiki burudani ya uhakika.”
Kavishe
 aliongeza kuwa mechi hii ni maalum kwa ajili ya kuhitimisha kampeni ya 
Nani Mtani Jembe ambayo imeendeshwa kwa zaidi ya miezi miwili ikiwapa 
fursa mashabiki wa timu hizi kuchangia timu zao kila wanapoburudika na 
bia ya Kilimanjaro Premium Lager.
Kilimanjaro
 Premium Lager   ilitenga kiasi cha shilingi milioni 100 
zinazoshindaniwa na Simba na Yanga kupitia mashabiki wake na tarehe 21 
Desemba ndio utakuwa mwisho wa kampeni ya Nani Mtani Jembe ambapo baada 
ya mechi  fedha hizo zitagawanywa kwa kila timu kulingana na matokeo ya 
kura za mashabiki na klabu zitajiamulia namna ya kutumia fedha hizo.
Kampeni
 hii imeleta msisimko mkubwa sana kati ya mashabiki na hadi sasa matokeo
 ya kampeni hii yanaonyesha kwamba Yanga wanaongoza wakiwa na kiasi cha 
shilingi milioni 76 huku Simba wakiwa na kiasi cha shilingi milioni 24
Mashabiki
 wa Simba na Yanga wanaoshiriki katika kampeni ya Nani Mtani Jembe 
wanaendelea kunufaika zaidi na zawadi kabambe zilizoandaliwa na bia ya 
Kilimanjaro Premium Lager ili kuongeza msisimko na ushiriki katika 
kampeni hiyo ambapo mashabiki watatu wa Simba na mashabiki watatu wa 
Yanga wanajishindia kiasi cha shilingi 300,000/= kila mmoja katika droo 
zinazofanyika mara moja kila wiki. Droo kubwa itafanyika tarehe 21 
Desemba.  Ambapo katika droo hiyo kubwa shilingi milioni 6 zitatolewa 
kama zawadi kwa washindi wawili –  mmoja shabiki wa Yanga na mwingine 
shabiki wa Simba ambapo kila mmoja atajishindia shilingi milioni tatu. 

No comments:
Post a Comment