Waziri
 wa Ujenzi, John Magufuli akisisitiza jambo alipokuwa akikagua ujenzi wa
 barabara, amewaonya makandarasi wasiofuta vigezo katika ujenzi wa 
barabara nchini kwamba hatasita kuwatimua 
Dar es Salaam.
 Waziri wa Ujenzi, John Magufuli amewaonya makandarasi waliopewa kazi ya
 ujenzi wa barabara kwenye Mikoa ya Dodoma, Manyara na Mtwara kutekeleza
 yaliyomo kwenye mkataba vinginevyo hatasita kuwashughulikia.
Magufuli
 aliyasema hayo jana kwenye hafla ya utiaji wa saini ujenzi wa barabara 
kwenye mikoa hiyo uliofanywa na Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) 
na kampuni za ujenzi na usimamizi kutoka China na Ujerumani wenye jumla 
ya Sh 539 bilioni.
“Kama
 mnaona hamtatekeleza yaliyomo kwenye mkataba kama vile ujenzi kuchelewa
 na kujenga chini ya kiwango, tafadhali msisaini mkataba huu kwa sababu 
mtapata shida,” alisema.
Magufuli
 alisema fedha za ujenzi wa barabara hizo ni mkopo kutoka Benki ya 
Maendeleo ya Afrika (AfDB) ambao wametoa asilimia 65 ya kiasi hicho na 
Wakala wa Ushiriano wa Kimataifa wa Japan (Jica) waliotoa asilimia 29 
wakati serikali imetoa asilimia tano.
Aliwaagiza
 watendaji wakuu wa Tanroads waliopo kwenye mikoa ya miradi hiyo 
kusimamia ipasavyo ujenzi wa barabara hizo vinginevyo watahesabika kama 
wameshindwa kazi. Aidha, Magufuli aliwataka Tanroads kufuata sheria 
kuwashughulikia wenye malori wanaozidisha uzito kwani hao ndiyo 
wanaosababisha uharibifu wa barabara zinazojengwa kwa gharama kubwa.
Miradi iliyosainiwa jana 
Mtendaji
 Mkuu wa Tanroads, Patrick Mfugale alisema mradi wa ujenzi wa kati ya 
Mayamaya hadi Meela ambazo ni kilometa 99.35 mkoani Dodoma itajengwa na 
kampuni ya China Henan International Cooperation Group kwa gharama ya Sh
 100.1 bilioni.
Alisema kazi ya usimamizi wa mradi huo imepewa kampuni ya Crown Tech-Consult Ltd ya Tanzania kwa gharama ya Sh2.7 bilioni.
Alisema
 mkataba wa ujenzi wa barabara kati ya Meela hadi Bonga kwa upande wenye
 kilomita 88.8 umesainiwa na Kampuni ya China Railways Seventh Group Co.
 Ltd kwa gharama ya Sh88.3 bilioni tekelezaji ni miezi 36 kuanzia jana.
“Usimamizi
 wa mradi huo imepewa kampuni ya HP Gauff Inginieure GMBH na KG-JBG ya 
Ujerumani kwa gharama za Euro 2, 357,200 sawa na Sh 4.9 bilioni.
Mfugale
 alisema mkataba wa ujenzi kati ya Mangaka hadi Mtambaswala mkoani 
Mtwara ambazo ni kilometa 65.5 imepewa Kampuni ya Sichuan Road and 
Bridge Group Cooperation Ltd ya China.
Alisema kampuni hiyo itajenga kipande hicho kwa gharama ya Sh 60 bilioni na kwamba utekelezaji wake ni miezi 24.
Mfugale
 alisema zabuni za ujenzi wa barabara hizo zilitangazwa Novemba Mosi, 
2012 na kwamba kampuni 187 zilijitokeza kuomba kazi hiyo.
CHANZO: MWANANCHI

No comments:
Post a Comment