TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, December 3, 2013

Waziri Magufuli awashukia makandarasi

Waziri wa Ujenzi, John Magufuli akisisitiza jambo alipokuwa akikagua ujenzi wa barabara, amewaonya makandarasi wasiofuta vigezo katika ujenzi wa barabara nchini kwamba hatasita kuwatimua
Dar es Salaam. Waziri wa Ujenzi, John Magufuli amewaonya makandarasi waliopewa kazi ya ujenzi wa barabara kwenye Mikoa ya Dodoma, Manyara na Mtwara kutekeleza yaliyomo kwenye mkataba vinginevyo hatasita kuwashughulikia.
Magufuli aliyasema hayo jana kwenye hafla ya utiaji wa saini ujenzi wa barabara kwenye mikoa hiyo uliofanywa na Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) na kampuni za ujenzi na usimamizi kutoka China na Ujerumani wenye jumla ya Sh 539 bilioni.
“Kama mnaona hamtatekeleza yaliyomo kwenye mkataba kama vile ujenzi kuchelewa na kujenga chini ya kiwango, tafadhali msisaini mkataba huu kwa sababu mtapata shida,” alisema.
Magufuli alisema fedha za ujenzi wa barabara hizo ni mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) ambao wametoa asilimia 65 ya kiasi hicho na Wakala wa Ushiriano wa Kimataifa wa Japan (Jica) waliotoa asilimia 29 wakati serikali imetoa asilimia tano.
Aliwaagiza watendaji wakuu wa Tanroads waliopo kwenye mikoa ya miradi hiyo kusimamia ipasavyo ujenzi wa barabara hizo vinginevyo watahesabika kama wameshindwa kazi. Aidha, Magufuli aliwataka Tanroads kufuata sheria kuwashughulikia wenye malori wanaozidisha uzito kwani hao ndiyo wanaosababisha uharibifu wa barabara zinazojengwa kwa gharama kubwa.
Miradi iliyosainiwa jana
Mtendaji Mkuu wa Tanroads, Patrick Mfugale alisema mradi wa ujenzi wa kati ya Mayamaya hadi Meela ambazo ni kilometa 99.35 mkoani Dodoma itajengwa na kampuni ya China Henan International Cooperation Group kwa gharama ya Sh 100.1 bilioni.
Alisema kazi ya usimamizi wa mradi huo imepewa kampuni ya Crown Tech-Consult Ltd ya Tanzania kwa gharama ya Sh2.7 bilioni.
Alisema mkataba wa ujenzi wa barabara kati ya Meela hadi Bonga kwa upande wenye kilomita 88.8 umesainiwa na Kampuni ya China Railways Seventh Group Co. Ltd kwa gharama ya Sh88.3 bilioni tekelezaji ni miezi 36 kuanzia jana.
“Usimamizi wa mradi huo imepewa kampuni ya HP Gauff Inginieure GMBH na KG-JBG ya Ujerumani kwa gharama za Euro 2, 357,200 sawa na Sh 4.9 bilioni.
Mfugale alisema mkataba wa ujenzi kati ya Mangaka hadi Mtambaswala mkoani Mtwara ambazo ni kilometa 65.5 imepewa Kampuni ya Sichuan Road and Bridge Group Cooperation Ltd ya China.
Alisema kampuni hiyo itajenga kipande hicho kwa gharama ya Sh 60 bilioni na kwamba utekelezaji wake ni miezi 24.
Mfugale alisema zabuni za ujenzi wa barabara hizo zilitangazwa Novemba Mosi, 2012 na kwamba kampuni 187 zilijitokeza kuomba kazi hiyo.
CHANZO: MWANANCHI

No comments:

Post a Comment