TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, December 1, 2013

Wachina wasaidia watoto yatima


Mama_Anna_Mkapa
Kibaha. Mwenyekiti wa mfuko wa fursa sawa kwa wote, Mama Anna Mkapa ametoa wito kwa jamii kushiriki kuwasaidia watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu ili kupata mahitaji yao muhimu kama walivyo wengine.
Mama Mkapa alitoa wito huo jana Mjini Kibaha wakati akipokea msaada wa vitu mbalimbali vyenye thamani ya Sh7 milioni vilivyotolewa na Umoja wa Wafanyabiashara wa China kwenye kijiji cha kulelea watoto yatima Kibaha.
Akizungumza wakati akipokea msaada huo, alisema kuna haja ya kila mtu kusaidia watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu ili waweze kuishi kwenye vizuri kama walivyo watoto wenye wazazi.
“Naomba kila mtu na kila jamii itambue umuhimu wa kuwasaidia watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, kwani watoto hawa ni wetu sote,” alisema Mama Mkapa.
Mama Mkapa alishukuru umoja huo kwa kutoa msaada huo ambao utasaidia kuongeza nguvu kwenye kituo hicho.
Naye mwakilishi wa Umoja huo wa wafanyabiashara hao Wachina, Hu- Jianxi alisema kuwa wameguswa kuwasaidia watoto hao kwani wanahitaji kusaidiwa ili nao wajisikie kama jamii za watoto wengine wanaolelewa na wazazi wao.

No comments:

Post a Comment