Kibaha.
 Mwenyekiti wa mfuko wa fursa sawa kwa wote, Mama Anna Mkapa ametoa wito
 kwa jamii kushiriki kuwasaidia watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu
 ili kupata mahitaji yao muhimu kama walivyo wengine.
Mama
 Mkapa alitoa wito huo jana Mjini Kibaha wakati akipokea msaada wa vitu 
mbalimbali vyenye thamani ya Sh7 milioni vilivyotolewa na Umoja wa 
Wafanyabiashara wa China kwenye kijiji cha kulelea watoto yatima Kibaha.
Akizungumza
 wakati akipokea msaada huo, alisema kuna haja ya kila mtu kusaidia 
watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu ili waweze kuishi kwenye vizuri
 kama walivyo watoto wenye wazazi.
“Naomba
 kila mtu na kila jamii itambue umuhimu wa kuwasaidia watoto wanaoishi 
kwenye mazingira magumu, kwani watoto hawa ni wetu sote,” alisema Mama 
Mkapa.
Mama Mkapa alishukuru umoja huo kwa kutoa msaada huo ambao utasaidia kuongeza nguvu kwenye kituo hicho.
Naye
 mwakilishi wa Umoja huo wa wafanyabiashara hao Wachina, Hu- Jianxi 
alisema kuwa wameguswa kuwasaidia watoto hao kwani wanahitaji kusaidiwa 
ili nao wajisikie kama jamii za watoto wengine wanaolelewa na wazazi 
wao.

No comments:
Post a Comment