TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, December 3, 2013

Lowassa ammwagia sifa Mkapa

Lowassa 
Masasi. Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa amemmwagia sifa Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa kuwa ni kiongozi aliyeliongoza taifa kwa uadilifu na umakini.
Lowassa aliyasema hayo mwishoni mwa wiki mjini Masasi mkoani Mtwara katika harambee ya kuchangia shughuli za maendeleo za Ushirika wa Mama wa Kikristo (UMAKI) katika Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Masasi,
“Nimefika hapa kwa heshima. Nimefika hapa Masasi kutokana na kwamba wilaya hii imetoa kiongozi, Rais Benjamin Mkapa aliyeliongoza taifa kwa umakini, uadilifu na ushupavu mkubwa.
Lowassa ambaye wakati wa uongozi wa Serikali ya Mkapa alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira na Muungano) kabla ya kupelekwa Wizara ya Maji na Mifugo, alisema lazima Watanzania wampe heshima yake na kumuenzi kutokana na kile alichokifanya kwa Taifa.
Mbali na hayo, Lowassa alisema yuko tayari kushirikiana na mtu yeyote mwenye nia ya dhati ya kupambana kuondoa umaskini katika jamii kwa kuwa yeye ni mdau wa wanaopambana na kuondoa umaskini katika jamii.
“Mtu yoyote anayepambana na kuondoa umaskini katika jamii, kwa kweli mtu huyo niko tayari kushirikiana naye katika harambee za harakati hizo,” alisema Lowassa na kuongeza kuwa wanawake ni jamii inayochukia umaskini.
“Wanawake ni wadau wakubwa katika kupambana na umaskini, na ndiyo maana chama changu cha CCM katika Rasimu ya Katiba Mpya inataka kuwe na asilimia 50 kwa 50 ya uwakilishi bungeni na kwamba chama hicho kinawathamini sana kinamama wote nchini.
Aidha, katika harambee hiyo, zaidi ya Sh103 milioni zilipatikana huku marafiki zake wakichangia Sh10 millioni na kuvuka lengo ambalo lilikuwa Sh100 milioni.
 CHANZO: MWANANCHI

No comments:

Post a Comment