Masasi.
 Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa amemmwagia 
sifa Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa kuwa ni kiongozi 
aliyeliongoza taifa kwa uadilifu na umakini.
Lowassa
 aliyasema hayo mwishoni mwa wiki mjini Masasi mkoani Mtwara katika 
harambee ya kuchangia shughuli za maendeleo za Ushirika wa Mama wa 
Kikristo (UMAKI) katika Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Masasi,
“Nimefika
 hapa kwa heshima. Nimefika hapa Masasi kutokana na kwamba wilaya hii 
imetoa kiongozi, Rais Benjamin Mkapa aliyeliongoza taifa kwa umakini, 
uadilifu na ushupavu mkubwa.
Lowassa
 ambaye wakati wa uongozi wa Serikali ya Mkapa alikuwa Waziri wa Nchi 
Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira na Muungano) kabla ya kupelekwa 
Wizara ya Maji na Mifugo, alisema lazima Watanzania wampe heshima yake 
na kumuenzi kutokana na kile alichokifanya kwa Taifa.
Mbali
 na hayo, Lowassa alisema yuko tayari kushirikiana na mtu yeyote mwenye 
nia ya dhati ya kupambana kuondoa umaskini katika jamii kwa kuwa yeye ni
 mdau wa wanaopambana na kuondoa umaskini katika jamii.
“Mtu 
yoyote anayepambana na kuondoa umaskini katika jamii, kwa kweli mtu huyo
 niko tayari kushirikiana naye katika harambee za harakati hizo,” 
alisema Lowassa na kuongeza kuwa wanawake ni jamii inayochukia umaskini.
“Wanawake
 ni wadau wakubwa katika kupambana na umaskini, na ndiyo maana chama 
changu cha CCM katika Rasimu ya Katiba Mpya inataka kuwe na asilimia 50 
kwa 50 ya uwakilishi bungeni na kwamba chama hicho kinawathamini sana 
kinamama wote nchini.
Aidha,
 katika harambee hiyo, zaidi ya Sh103 milioni zilipatikana huku marafiki
 zake wakichangia Sh10 millioni na kuvuka lengo ambalo lilikuwa Sh100 
milioni.
 CHANZO: MWANANCHI

No comments:
Post a Comment