TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, December 3, 2013

OKWI , KIIZA WAIFUMUA ERITREA 3-0,


Emmanuel-Okwii 
Jembe la kazi la zamani la Simba Sc: Emmanuel Anord Okwi, leo hii amefunga mawili katika mchezo muhimu wa CECAFA dhidi ya Eritrea na kupanda kileleni mwa kundi C
……………………………………………………………………………
Na Baraka Mpenja 

MECHI za kundi C za kombe la Mataifa ya Afrika mashariki na kati, CECAFA Challenge, zimeendelea leo ambao Mabingwa watetezi wa kombe hilo, Timu ya Taifa ya Uganda imejihakikisha kutinga robo fainali baada ya kuifumua Eritrea mabao 3-0, Uwanja wa City, jijini Nairobi, Kenya.
Mabao ya Uganda leo hii yalifungwa na nyota wa zamani wa wekundu wa Msimbazi Simba Sc, Emmanuel Anord Okwi aliyepiga mawili katika dakika ya 9 na 39, huku moja likitiwa kambani na `Diego wa Kampala`, Khamis Friday Kiiza anayecheza Yanga ya Dar es salaam kwa mkwaju wa penati dakika ya 19 ya mchezo.
Ushindi huo unaifanya Uganda ifikishe pointi 6 kutokana na matokeo ya awali ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Amavubi na kupanda kileleni mwa kundi hilo kwa wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa, kwani hata Sudan wanazo alama 6 kibindoni.
Mchezo wa mapema uliwakutanisha Rwanada na Sudan na kushuhudia Amavubi wakila `nakozi` ya bao 1-0 tena kutoka kwa Sudan.
Matokeo hayo ni mabaya zaidi kwa Rwanda huku Nahodha wake, Haruna Niyonzima akishikwa na machungu zaid kutokana na mchezaji mwenzake wa Yanga, Khamis Kiiza kuendelea kudunda kwa raha zake.
Bao hilo pekee na muhimu zaidi kwa Sudan limefungwa katika dakika ya 29 kupitia kwa Salah Ibrahim.
Matokeo ya leo yanaiweka Rwanda katika mazingira magumu ya kusonga mbele hatua ya robo fainali kwani mchezo wa awali walikalia cha mtema kuni baada ya kulambishwa bao 1-0 na Uganda.
Katika kundi A, wenyeji Harambee Stars na wahabeshi wa Ethiopia wapo nafasi nzuri ya kwenda robo fainali na Zanzibar heroes inayoshika nafasi ya tatu, inaweza kuangukia katika kuwania moja ya nafasi mbili za best losers.
Iwapo Zanzibar itaifumua Harambee Stars  watawania Robo Fainali katika nafasi mbili za best loosers.
Kundi B Zambia imejihakikishia kwenda Robo Fainali na mechi baina ya Tanzania Bara na Burundi itaamua timu ya kuungana na mabingwa hao wa zamani wa Afrika na ya kuwania kufuzu kwa nafasi za best losers.      
Michuano hiyo itaendelea kesho kwa timu za kundi A kushuka dimbani kuwania mzigo wa pointi tatu muhimu.
Mechi ya mapema itawakutanisha Sudan Kusini dhidi ya Ethiopia, wakati wenyeji wa michuano ya mwaka huu, timu ya Taifa ya Kenya, Harambee Stars itamenyana na mashujaa wa visiwani, Zanzibar Heroes.

No comments:

Post a Comment