Jembe
 la kazi la zamani la Simba Sc: Emmanuel Anord Okwi, leo hii amefunga 
mawili katika mchezo muhimu wa CECAFA dhidi ya Eritrea na kupanda 
kileleni mwa kundi C
……………………………………………………………………………
Na Baraka Mpenja 
MECHI
 za kundi C za kombe la Mataifa ya Afrika mashariki na kati, CECAFA 
Challenge, zimeendelea leo ambao Mabingwa watetezi wa kombe hilo, Timu 
ya Taifa ya Uganda imejihakikisha kutinga robo fainali baada ya kuifumua
 Eritrea mabao 3-0, Uwanja wa City, jijini Nairobi, Kenya.
Mabao
 ya Uganda leo hii yalifungwa na nyota wa zamani wa wekundu wa Msimbazi 
Simba Sc, Emmanuel Anord Okwi aliyepiga mawili katika dakika ya 9 na 39,
 huku moja likitiwa kambani na `Diego wa Kampala`, Khamis Friday Kiiza 
anayecheza Yanga ya Dar es salaam kwa mkwaju wa penati dakika ya 19 ya 
mchezo.
Ushindi
 huo unaifanya Uganda ifikishe pointi 6 kutokana na matokeo ya awali ya 
ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Amavubi na kupanda kileleni mwa kundi hilo 
kwa wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa, kwani hata Sudan 
wanazo alama 6 kibindoni.
Mchezo wa mapema uliwakutanisha Rwanada na Sudan na kushuhudia Amavubi wakila `nakozi` ya bao 1-0 tena kutoka kwa Sudan.
Matokeo
 hayo ni mabaya zaidi kwa Rwanda huku Nahodha wake, Haruna Niyonzima 
akishikwa na machungu zaid kutokana na mchezaji mwenzake wa Yanga, 
Khamis Kiiza kuendelea kudunda kwa raha zake.
Bao hilo pekee na muhimu zaidi kwa Sudan limefungwa katika dakika ya 29 kupitia kwa Salah Ibrahim.
Matokeo
 ya leo yanaiweka Rwanda katika mazingira magumu ya kusonga mbele hatua 
ya robo fainali kwani mchezo wa awali walikalia cha mtema kuni baada ya 
kulambishwa bao 1-0 na Uganda. 
Katika
 kundi A, wenyeji Harambee Stars na wahabeshi wa Ethiopia wapo nafasi 
nzuri ya kwenda robo fainali na Zanzibar heroes inayoshika nafasi ya 
tatu, inaweza kuangukia katika kuwania moja ya nafasi mbili za best 
losers. 
Iwapo Zanzibar itaifumua Harambee Stars  watawania Robo Fainali katika nafasi mbili za best loosers.
Kundi B Zambia imejihakikishia kwenda Robo Fainali na mechi baina ya Tanzania Bara na Burundi itaamua timu ya kuungana na mabingwa hao wa zamani wa Afrika na ya kuwania kufuzu kwa nafasi za best losers.
Kundi B Zambia imejihakikishia kwenda Robo Fainali na mechi baina ya Tanzania Bara na Burundi itaamua timu ya kuungana na mabingwa hao wa zamani wa Afrika na ya kuwania kufuzu kwa nafasi za best losers.
Michuano hiyo itaendelea kesho kwa timu za kundi A kushuka dimbani kuwania mzigo wa pointi tatu muhimu.
Mechi
 ya mapema itawakutanisha Sudan Kusini dhidi ya Ethiopia, wakati wenyeji
 wa michuano ya mwaka huu, timu ya Taifa ya Kenya, Harambee Stars 
itamenyana na mashujaa wa visiwani, Zanzibar Heroes.

No comments:
Post a Comment