TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, December 3, 2013

UWT ZANZIBAR: VIKUNDI VYA KINANA VINASAIDIWA FEDHA LAKINI VINAATHIRIWA NA DIRA MBOVU YA KUVIENDELEZA

Naibu Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar Bi. Salama Abuud Talib akimkaribisha Makamu Mwenyekiti UWT Bi. Asha Bakari Makame kuzungumza na wandishi wa Habari kuhusu miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa upande wa Jumuiya hiyo. 02-4 
Makamu Mwenyekiti UWT Bi. Asha Bakari Makame akizunguza na wandishi wa Habari kuhusu miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar. 03-2 
Makamu Mwenyekiti UWT Bi. Asha Bakari Makame akisisitiza kitu alipokuwa akizungumza na wandishi wa Habari kuhusu miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar ofisini Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini
Zanzibar.
 04-3Mwandishi wa Habari wa Chuchu Fm Radio Rahama Suleiman akitaka ufafanuzi wa kitu kwenye Mkutano wa UWT ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar.
(Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).
Na Ali Issa Maelezo-Zanzibar
Umoja wa wanawake wa CCM Tanzania (UWT) umesema vikundi vingi vya ushirika vya kina mama vimesaidiwa  fedha nyingi za mikopo kujiendesha lakini inaonekana bado kuna baadhi ya kinamama wanashindwa kuviendesha vikundi hivyo kutokana na kutokuwa na dira nzuri kuviendeleza vikundi hivyo.
Hayo yamesemwa leo huko ofisi kuu ya Chama cha Mapinduzi Kisiwandui Mjini Zanzibar na Naibu Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar Salama Aboud Talib wakati alipokuwa na mazungumzo na waandishi wa Habari katika kuadhimisha sherehe za miaka 50 ya mapinduzi Zanzibar kwa Jumuiya ya wanawake wa CCM Zanzibar.
Amesema umoja wa wanawake Tanzania  kupitia wake wa viongozi wa kuu wa Serikali na tasisi nyengine wametoa  pesa nyingi katika kusaidia vikundi vya kinamama ili kujikwamua na umasini na kuviendeleza vikundi vyao kupata tija jambo ambalo baadhi ya viongozi  wa vikundi hivyo hushindwa kuviendeleza na hatimae kutofikia malengo ya kuazishwa kwake.
Amesema hali hiyo si njema kwani inarudisha nyuma juhudi za viongozi jambo ambalo lengo la chama cha Mapinduzi ni kuijenga jamii ya wanawake kua na muelekeo mzuri kimaendeleo na kujinasua na umasikini.
“Wake waviongozi wetu huwapa pesa nyingi wana vikundi  kuwasaidia wanawake   lakini vikundi hivyo hushindwa kuziendeleza pesa zile na baadae kikundi huwa kina shindwa kujiendeshana pesa kupotea,” alisema Salama.
Aidha alifahamisha kuwa wanashindwa kufahamu kupotea kwa pesa hizo kwani amesema kabla ya kutolewa peasa hizo vikundi hupatiwa mafunzo kutoka kwa wataalamu ili waweze kuviendesha.
Bi.Salama alisema hali hiyo haifurahishi hata kidogo kuona pesa zinapotea na vikundi kufa na italazimika kwa wanavikundi kutafuta mbinu mbadala badala ya zile za kitalamu ili kuona vikundi vina piga hatukubwa za kimaendeleo.
Nae Makamo mwenyekiti UWT Bi. Asha Bakari Makame alisikitishwa sana na suala la unyanyasaji kwa watoto na wanawake na kuishauri Serikali iangalie kwa umakini suala hilo kwani inaonekana kuna mtandao mkubwa wa kuwadhalilisha watoto kwa kuwanajisi hali ambayo ni hatari katika taifa hili la Zanzibar.
Amesema Serikali iangalie sheria zake na kuzifanyia marekebisho kwani watoto wanaharibiwa vibaya na watuhumiwa kushindwa kuingia hatiani jambo ambalo sisahihi kwa watoto kudhalilishwa kwa kunajiwa na kutengwa na wazaziwao. 
Makamo huyo alisifu juhudi za Jumuiya hiyo inazochukua kwa kua karibu na wana nchi kupitia Serikali kuu kwa kufuata ilani ya chama cha Mapinduzi.
Alisema hivi sasa wanawake wa Zanzibar wamefaidika sana na Jumuiya hiyo kwa kupata frusa katika ngazi za Sekikali na kuweza pia kupata elimu na ajira kwa idadi ya wanawake ambayo ni wazi kuwa wanwake wa Zanibar wanathaminiwa sana na serikali yao.
Bi.Asha Bakari alizipongeza Serikali zilizo pita,Viongozi wa Afroshirazi na hii ilioko madarakani kwa kuyaendeleza Mapinduzi matukufu yalio mkomboa mwanamke kutoka katika utwala wakisultani na 1964 kua Taifa  huru,lenye  Umoja amani na mshikamano.

No comments:

Post a Comment