Na Mussa Mkama
MKURUGENZI
 Mtendaji wa Msama Promitions Alex Msama amekabidhi msaada wa magodoro 
yenye dhamani ya zaidi ya Shilingi milioni 4 kwa kituo cha watoto yatima
 Luhila Pachane kilichopo Songea Mkoani Ruvuma.
![]()  | 
| Alex Msama | 
Akizungumza
 na waandishi wa habari katika makao makuu ya ofisi za Msama Promotions 
Kinondoni Jijini Dar es Salaam jana Msama alisema msaada huo umetoka 
kwenye mfuko wa Tamasha la Krismas ambalo linatarajiwa kuanza Desemba 25
 jijini hapa na mikoa mingine.
Tamasha hilo la Krismas linatarajia kufanyika katika mikoa mitano, ambapo ni Dar es Salaam, Morogoro, Tanga, Arusha na Dodoma.
Msama
 alisema kuwa kutokana na maombi ya kituo hicho na kuguswa na hali 
waliyokuwa nayo ya yatima hao kulala katika mkeka, aliamua kunyofoa 
sehemu ya fedha zilizokuwa kwenye mfuko wa Tamasha la Krismas na kuamuo 
kuwasaidi watoto hao ili nao waweze kujisikia wapo katika jamii ya 
Watanzania.
“Nimeamua
 kufanya hivyo kutokana na kuguswa na hali halisi waliyonayo yatima hao 
wa kituo cha Luhila Pachane huko mkoani Ruvuma nikaamua kunyofoa fedha 
katika mfuko wa Tamasha la Krismas kwa ajili ya kuwasaidi ili nao 
wajisikie wako pamoja na Watanzania wenzao” alisema Msama na kuongeza 
kuwa;
“Msaada
 huo wa magodoro hayo ni zaidi ya shilingi milioni 4, hivyo ninaimani 
kubwa sasa kwa msaada huu yatima wataniombea kwa Mungu ili Tamasha la 
Krismas liwe la mafanikio kwani lengo la tamasha hilo ni kuweza kujenga 
kituo cha kisasa cha watoto yatima na wasiojiweza kwani kiwanja 
tumeshakiona kipo pale maeneo ya barabara ya Pugu Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza
 baada ya kukabidhiwa msaada huo Mlezi wa kituo hicho ambaye pia ni 
Katibu wa Bakwata mkoa wa Ruvuma Shekh Abdushakur Omary alisema 
anamshukuru Msama kwa wema wake aliouonyesha wa kusaidia jamii ya 
Watanzania wote bila kubagua dini, kabila wala rangi.
“Msama
 ni mtu wa aina yake hana ubaguzi anashughulikia maombi ya Watanzania 
wote bila kuangalia dini, kabila, rangi wala utaifa wake kwani amaamini 
kuwa wote ni wamoja, hivyo naomba nizidi kumuombea aendelee kuwa na moyo
 huo wa kujitolea kwa ajili ya watu wa taifa lake wasiyojiweza” alisema 
Omary.
Hata
 hivyo aliomba Wizara husika kuharakisha upatikanaji wa hati ya kiwanja 
kile kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha kisasa cha kutolea misaada 
(Center)  pamoja na kiwanda cha kisasa cha kuzalishia kazi za wasanii 
 kwa manufaa ya Taifa na watu wake, kwani kwa kufanya hivyo itakuwa 
imesaidia Watanzania wengi wenye ndoto ya kuwa wasanii wakubwa nchini.
“Uwepo
 wa Msama katika ulimwengu huu kunamuwakilisha Mwenye Mungu, kwani Mungu
 si mbaguzi kwa watu wake anawapenda wote na anatoa sawa kwa kila mtu, 
hivyo ndivyo alivyo Msama, kwa moyo mmoja namuombea yeye na taasisi yake
 isiyokuwa na ubaguzi wa dini kuendelea kuwa hivyo wakati wote” alisema 
Omari na kuongeza kuwa;
“Naomba
 Wizara au Waziri husika kuona umuhimu wa ujenzi wa kituo hicho cha 
kisasa cha kutolea misaada pamoja na kiwanda cha kuzalishia kazi za wasanii,
 kwani wapo Watanzania wengi wenye vipaji lakini hushindwa kufanya kazi 
za kisanii kutokana na viwanda kuwa na gharama kubwa wasizoweza 
kuzimudu” 

No comments:
Post a Comment