TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, December 2, 2013

MEREKEBISHO UWANJA WA SOKOINE MBEYA YAANZA KWA KASI KUBWA,


SAM_0720Na Baraka Mpenja -Dar es salaam
Wamiliki wa uwanja wa kumbukumbu ya sokoine jijini Mbeya wameanza rasmi mchakato wa kufanyia marekebisho uwanja huo kama walivyoagizwa na shirikisho la soka Tanzania TFF.
Meneja wa uwanja huo, Modestus Mbande Mwaluka amesema ndani ya wiki mbili watakuwa wamekamilisha marekebisho na baada ya hapo wataanza kumwagilia maji sehemu ya pichi.
“Jana tumeanza kwa kung`oa magoli, leo tunaanza kushughulikia sehemu ya ndani ya uwanja, magreda yameshaagizwa na lazima yaje ili kuutifua na kupanda nyasi mpya. Kizuri pesa ipo ndugu yangu”. Alisema Mwaluka.
“Kizuri zaidi hiki ni kipindi cha mvua jijini hapa, itasaidia sana ukizingatia uwepo wa maji ya bomba. Nyasi zitakua haraka na kubadili mandhari ya uwanja huu”.
Mwaluka amesema wanataka uwanja huo uwe mzuri na utumike katika michuano ya kimataifa, na kwasasa watarekebisha miundo mbinu yote ikiwemo vyumba vya kubadilishia nguo kwa wachezaji, vyoo na maeneo mengine muhimu.
IMG-20120915-WA0005
“Ujue tulishasema kutoka mwanzo kuwa, tupo katika mkakati madhubuti wa kuufanya uwanja wetu uwe bora, tulianza na uzio, tumeshaimarisha, sasa tunafuata sehemu ya ndani `Pitch`, tutafuata vyumba vya kubadilishia nguo, halafu vyoo na miondombinu mingine”. Aliongeza mwaluka.
Meneja huyo alisitiza kuwa wapenda michezo jijini Mbeya ambao ni mashabiki wa timu za Mbeya  City na Tanzania Prisons wasiwe na wasiwasi kwani timu zao zitatumia uwanja huo, na kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa ligi kuu januari 25, uwanja utakuwa bora”. Alisema Mwaluka.
Endapo uwanja huo hautarekebishwa kwa haraka, timu mbili za ligi kuu Mbeya City na Tanzania Prisons zipo hatarini kucheza nje ya Mbeya, kitendo ambacho kitawanyima fursa kuzishangilia timu zao kwa wingi.

No comments:

Post a Comment