TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, December 3, 2013

Wagonjwa wa moyo wapata ufadhili kwenda India kutibiwa


Wagonjwa watano wenye maradhi mbalimbali ya moyo wamekwenda nchini India kwa matibabu ambapo wengine watafanyiwa upasuaji.
Wagonjwa hao ambao wanatarajiwa kurejea nchini baada ya wiki nne, wamefadhiliwa kwa pamoja na Hospitali ya Regency Medical Center, Lions Club ya Dar es Salaam (Host), Lions club ya Arusha na  Prime Bank ya Kenya.
RegencyShughuli ya kuwaaga wagonjwa hao ilifanyika juzi jioni katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ambapo ilihudhuriwa na Rais wa Lions,  Nureen Nathoo, Rais wa zamani wa Lions, Shiraz Rashid, Mwenyekiti wa kanda wa Lions, Lion Bakary Omary na mratibu wa maradhi ya moyo katika klabu ya Lions, Dk. Rajni Kanabar.
Kwa mujibu wa Dk. Kanabar, wagonjwa hao watatibiwa katika hospitali ya CIMS iliyoko mji wa Ahmedabad nchini India kwa punguzo ya gharama ya Dola 2,500 za Marekani.
“Tunawashukuru wasamaria wema wote waliofanikisha shughuli hii ikiwemo benki ya Kenya ambayo imetoa dola 5,000 kwenye mradi wa kupeleka wagonjwa nje,” alisema.
Dk. Kanabar alisema fedha hizo zitatumika katika upasuaji wa mgonjwa mmoja, tiketi na Dola 200 zitatolewa kwa wagonjwa wote ili ziwasaidie katika maisha wakiwa ugenini.
Dk. Kanabar alisema tangu kuanzishwa kwa mradi huo, watoto zaidi ya 2,500, vijana na watu wazima wamepelekwa nje kwa ajili ya matibabu ya moyo.
Gilda Sangwe, ambaye mtoto wake ana tundu kwenye moyo, aliwahsukuru watu waliojiotolea fedha kwa ajili ya wagonjwa hao kwani bila hivyo wasingemudu gharama.
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment