TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, December 1, 2013

Wawekezaji wa nyumba waunda umoja

59f0National-Housing-Corporation-NHC
Dar es Salaam. Wawekezaji wa Sekta ya miliki ya nyumba, wameunda umoja wao kwa kushirikiana na Shirika la Nyumba la Taifa(NHC).
Akitoa ufafanuzi kuhusu hatua ya kuanzisha umoja huo uliopewa jina la Chama cha Waendelezaji Miliki Tanzania, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba, (NHC), Nehemia Mchechu alisema kuwa huo ni mwanzo wa safari ya kuwa na muungano wa wawekezaji katika sekta hiyo wakishirikiana na Serikali.
Mchechu alisema wameanza na wawekezaji wakubwa 30, ambapo kadri siku zinavyokwenda anayetaka kujiunga atafanya hivyo.
Alisema umuhimu wa kuwa na muungano huo ni kuweza kuishauri Serikali kujenga kwa viwango badala ilivyo sasa kila mmoja anafanya kivyake.
Aidha, Mchechu alisema kuwa Tanzania wamechelewa kuanzisha umoja huo kwani mataifa mengi yameshafanya hivyo na kuzitolea mfano nchi za  Kenya, Uganda, Afrika ya Kusini na baadhi ya nchi Ulaya.
“Kwa umoja huu tutajenga imani kwa wateja wetu, ambao watakuwa na sehemu ya kukimbilia wanapoona mambo yanakwenda kinyume na matarajio,” alisema Mchechu.
Naye Mohamed Sharifu, Mtanzania anayeishi Dubai alisema kuwa amefurahishwa na hatua hiyo kwa kuwa itapunguza idadi ya majengo mabovu.

No comments:

Post a Comment