WASHINDI COPA COCA-COLA WAKABIDHIWA VITITA VYAO
Washindi wa Copa Coca-Cola 2014
wamekabidhiwa zawadi zao za fedha kutoka kwa mdhamini wa michuano hiyo
ya umri chini ya miaka 15 kwa wavulana na wasichana kampuni ya
Coca-Cola. Fedha hizo kwa washindi mbalimbali tayari zimeingizwa kwenye
akaunti zao.
Kwa upande wa wavulana; washindi
na kiwango walichopata ni mabingwa Dodoma (sh. milioni nane), makamu
bingwa Kinondoni (sh. milioni tano), mshindi wa tatu Kigoma (sh. milioni
tatu) wakati timu yenye nidhamu Tanga (sh. milioni moja).
Mchezaji bora Mwami Ismail kutoka
Kigoma (sh. 500,000), mfungaji bora Timoth Timoth wa Dodoma (sh.
500,000), kipa bora Kelvin Deogratia wa Geita (sh. 500,000) na mwamuzi
bora Abdallah Mbarome kutoka Zanzibar sh. 500,000).
Kwa upande wa wasichana ni
mabingwa Kinondoni (sh. milioni tano), makamu bingwa Ilala (sh. milioni
tatu), mshindi wa watatu Temeke (sh. milioni mbili) wakati timu yenye
nidhamu Mbeya imepata sh. milioni moja).
Zubeda Mohamed wa Kinondoni ambaye
ndiye mchezaji bora amepata sh. 500,000, mfungaji bora Stumai Abdallah
wa Temeke sh. 500,000 wakati kipa bora ni Suleta Saad wa Zanzibar sh.
500,000.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
No comments:
Post a Comment