TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, September 21, 2014

ABDULRAHMAN KINANA AMALIZA ZIARA YAKE JIMBO LA BAGAMOYO

1 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua maktaba ya shule ya mingi ya Jitegemee iliyopo kata ya Magomeni mjini Bagamoyo wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010, Kinana yupo katika ziara ya mikoa ya Pwani, Tanga na Iringa akiongozana na Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye. 3Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Mbunge wa jimbo la Bagamoyo  Dr. Shukuru Kawambwa akielekeza jambo wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Magomeni mjini Bagamoyo, Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Mh. Ahmde Kipozi. 4Mkuu wa mkoa wa Pwani Mh. Mwantumu Mahiza akizungumza jambo na mwenyekiti wa CCM mkoa wa Pwani Ndugu Mwinshehe Mlao. 5Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Pwani Ndugu Mwinshehe Mlao akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Jitegemee kata ya Magomeni mjini Bagamoyo. 7Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi waliojitokeza katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya shule ya msingi Jitegemee kata ya Magomeni Bagamoyo 8Baadhi ya wananchi waliohudhuria katika mkutano huo. 9Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Mbunge wa jimbo la Bagamoyo  Dr. Shukuru Kawambwa akiwahutubia wapiga kura wake hawapo pichani. 11 
Baadhi ya wanachama wapya wa CCM wakila kiapo mara baada ya kupokea kadi zao za uanachama wa CCM leo mjini Bagamoyo. 12 
Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi CCM Ndugu Nape Nnauye akitema cheche katika mkkutano huo.

No comments:

Post a Comment