TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, September 21, 2014

SERENGETI FIESTA YABISHA HODI MJINI MORO.

serengeti  SERENGETI BREWERIES LTD
RE: FOR IMMEDIATE RELEASE SERENGETI FIESTA YABISHA HODI MORO MJINI Morogoro-Tanzania-September 21st/2014   Wakati tamasha la Serengeti Fiesta likitimiza wiki ya saba huku likizunguka na wasanii katika mikoa mbalimbali ya Tanzania kutoa burudani ya aina yake, hakika kazi hiyo haikuwa rahisi kwani zaidi ya mikoa saba bado inalisubilia kwa hamu kubwa tamasha hilo la Serengeti Fiesta kwa mwaka 2014. Baada ya umati mkubwa kujitokeza katika mji wa Iringa, tamasha la Serengeti Fiesta sasa linabisha hodi mjini Morogoro, si kwa mikono mitupu bali likiwa na kundi la wasanii nyota zaidi ya 12 wa muziki wa kizazi kipya watakaopanda jukwaani hapo leo katika Uwanja wa Jamhuri. Tulipata nafasi ya kuzungumza na Stamina ambaye ni msanii wa muziki wa bongo fleva hapa mjini Morogoro naye alikuwa na haya ya kusema, “Nina furaha sana kwakuwa tamasha la Serengeti Fiesta litakuwa hapa mjini siku ya Jumapili na kama kawaida sitawaangusha mashabiki wangu. Nataka kuwapa shoo bora ambayo kamwe hawataisahau. Napenda kuwahakikishia kuwa msikose kuja katika shoo hii muhimu, njooni mmuone kijana wenu jukwaani akifanya mambo adimu. Mbali ya tamasha hilo, kutakuwa na matukio kadha wa kadha kama bonanza la soka na dansi la Fiesta ambapo washindi watapata fursa ya kutua Dar es Salaam kushuhudia shoo ya mwisho ya Serengeti Fiesta inayotarajiwa kufanyika Oktoba 18, mwaka huu. Wasanii wengine watakaotumbuiza katika tamasha hilo litakalofanyika katika Uwanja wa Jamhuri ni Afande Sele, Weusi, Ney wa Mitego, Vanessa, Linah, Young Killa, Bue, Makomando, Ommy Dimpoz, Mo Music, Baraka Da Prince, Y Tony na Joh Maker. “Tulikuwa na shoo yenye mafanikio makubwa mjini Iringa na ni matarajio yangu kwamba mashabiki wetu wa Morogoro watazidi wale wa Iringa pia napenda kutumia nafasi hii kuwahakikishia wakazi wa Morogoro na viunga vyake kuwa shoo kabambe itaporomoshwa na wasanii wakali wa muziki wa bongo fleva na mengine mengi mazuri kutoka na SBL, hivyo msikose,” alisema Rugambo Rodney-Brand Manager Serengeti Premium Lager Mwaka huu, tamasha la Serengeti Fiesta limevuta hisia za watu wengi toka katika kila kona ya mikoa yote ambayo tamasha hilo lilipita kwani watu wengi walijumuika nalo huku likiwa na kaulimbiu ‘Sambaza Upendo’ .

No comments:

Post a Comment