TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, September 21, 2014

JUMUIA YA WAZAZI YA ZINDUA VICOBA VYA MFANO ARUSHA.

JUMUIA ya wazazi ya Chama cha Mapinduzi, mkoa wa Arusha, imezindua rasmi  kikundi cha Vicoba cha mkoa huo kama kikundi cha mfano ili kuhamasisha wananchi kujiunga na kuanzisha Vikoba kila eneo ili kuinua hali zao za uchumi..
  Uamuzi huo wa kuanzisha Vikoba, ulifikiwa mwishoni mwa kikao cha baraza la wazazi mkoa kilichofanyika wilaya ya Karatu na kuazimia mkoa kuwa na kikundi ncha vikoba cha mfano ili kuvutia ngazi zingine za jumuia hiyo kuanzia wilaya hadi vijiji kuanzisha vikoba.
  Katibu wa jumuia ya wazazi mkoa wa Arusha, Daniel Mgaya, amesema katika kutekeleza maazimio ya kikao hicho cha baraza ,mkoa umeunda uongozio wa muda ikiwa ni hatua ya maandalizi ya kukamilisha katiba ya Vikoba, ili kuweza kuhudumia wanachama wake .
  Mgaya,amesema kupitia vikoba wanachama wataweza kubuni miradi mbalimbali ya kiuchumi nna hivyo kuboresha maisha yao na kwa kutambua kuwa vikoba ndio njia rahisi ya wananchi kuinua maisha.
 
   .Amesema kikao cha baraza kiliwateua, Lodamini Mollel, kuwa mwenyekiti,
Emanuel Loi Katibu, Aman Nassary kuwa mweka hazina ,huku Rehema Mohamed, Zaituni Kiobya Edward Seneu, Zakaria Mlyanga, na Josephine Shayo ,wakichaguliwa kuwa wajumbe .
  Mgaya,amesema kuwa pia baraza hilo la wazazi mkoa limemchagua, John Danil son Pallanyo,ambae ni mjumbe wa baraza hilo mkoa na taifa kusimamia mfuko huo.
  Amesema baraza limeweka  kiwango cha hisa cha shilingi 15,000, ambazo zitakuwa zikitolewa kila wiki ambapo mfuko wa jamii utachangiwa shilingi 150,000 kila wiki  mara tatu.
  .Lengo lakuanzishwa kwa vikoba ni kuinua maisha ya wanachama ,na kwa kupitia  kikundi hicho cha mkoa wanachama watakuwa na uwezo wa kubuni miradi ya kiuchumi na pia watapata  elimu ya ujasiriamali na hivyo kuboresha vikoba vitaklavyoanzishwa ngazi mbalimbali mkoani Arusha. .

No comments:

Post a Comment