Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo  cha Sheria na Haki za Binadamu, Dk.Helen Kijo-Bisimba.
Mratibu wa Dawati la Katiba LHRC, Anna Henga 
Mwanasheria wa LHRC,  Harold Sungusia
 Mkurugenzi
 Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Dk.Helen Kijo-Bisimba
 (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es 
Salaam jana, wakati akitoa taarifa kuhusu awamu ya pili ya kampeni ya 
kusambaza uelewa wa rasimu ya pili (Kampeni Gogota). Kulia ni Mratibu wa
 Dawati la Katiba wa kituo hicho, Anna Henga na Mwanasheria wa Kituo 
hicho, Harold Sungusia. (Imeandaliwa na mtandao wa habari za 
jamii.com-simu 0712-727062)
Wanahabari wakiwa kwenye mkutano huo.
Wanahabari wakiwa kwenye mkutano huo.
Dotto Mwaibale
KITUO cha
 Sheria na Haki za Binadamu kimedai kuwa Bunge Maalumu la Katiba 
linaloendelea linaendeshwa kimabavu kwa na kutumia fedha za wananchi 
bure wakati wakijua fika hakuna katiba itakayopatikana.
Hayo 
yalisemwa Dar es Salaam jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria 
na Haki za Binadam (LHRC) Dk. Helen Kijo-Bisimba, wakati akitoa taarifa 
kuhusu awamu ya pili ya kampeni ya kusambaza uelewa wa rasimu ya pili 
(Kampeni gogota) kwa wananchi.
“Cha 
kusikitisha ni kwamba tumepoteza mabilioni ya fedha ambazo zingeweza 
kusaidia kwenye sekta mbali mbali zikiwemo za afya na elimu kwa kuwalipa
 wajumbe wa bunge la katiba,” alisema.
Alisema 
wakati wa kampeni hiyo ambayo imefanyika kwenye mikoa 20 nchini kituo 
hicho kimebaini kuwa wapo asilimia kubwa ya wananchi wanakerwa na 
mwenendo wa mchakato wa bunge hilo kwa kuchakachua maoni yao 
yaliyokusanywa na Tume ya mabadiliko ya katiba.
Alisema 
wakati wa kampeni hiyo ya gogota kituo hicho kimefanikiwa kufika kwenye 
wilaya zote, na kata tatu kwa kila mkoa ambapo kilifanikiwa kurudisha 
ajenda ya katiba na uelewa wa rasimu ya pili ya katiba kwa wananchi.
Alisema 
hiyo ni moja ya mafanikio waliyoyapata kuyajua kwa wananchi kwenye 
kampeni hiyo ambayo ililenga kuhamasisha wananchi kushiriki katika 
mchakato hususani kufuatilia bunge la katiba na upigaji wa kura ya maoni
 muda utakapo fika.
Pamoja na
 mafanikio hayo pia kitu hicho kimekutana na changamoto mbali mbali 
ikiwemo ya uelewa mdogo kuhusu katiba hususani walio pembezoni mwa miji.
Alitaja 
mikoa hiyo ni Arusha, Tanga, Kagera, Geita, Mwanza, Simiyu, Mbeya, 
Rukwa, Kilimanjaro, Manyara, Katavi, Iringa, Mara, Njombe, Ruvuma, Pemba
 Kaskazini, Kusini, Pemba mjini Magharibi, Unguja Kusini na Kasazini.
Alitaja 
changamoto nyingine ni kutokujua kusoma na kuandika kwa baadhi ya 
wananchi, umangi meza kwa badhi ya viongozi wa mikoa, hofu ya kutopata 
katiba na mfumo dume kwenye jamii.
No comments:
Post a Comment