Ukosefu wa Uwazi ni Chanzo cha Rushwa
Kipimo Abdallah
KUTOKUWEPO kwa uwazi, uadilifu 
na uwajibikaji katika mikataba mbalimbali ambayo serikali inaingia na 
wawakezaji kutoka nje ni moja ya sababu ya kuongezeka kwa rushwa kwa 
baadhi ya watumishi wa umma na wawekezaji.
Hayo yamebainishwa na Mwahadhiri
 Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Idara ya Uchumi 
Profesa Humphrey Moshi wakati akizungumza na mwandishi habari hii kwenye
 kongamano ambalo linaratibiwa na taasisi ya Jukwaa la Sera (Policy 
Forum).
Alisema kukosekana kwa  uwazi 
katika  mikataba mbalimbali ni moja ya sababu ambayo imekuwa ichangia 
rushwa kwenye michakato na makubaliano mengi ambayo yanahusisha serikali
 na wawakezaji.
Profesa Mushi alisema Serikali 
imekuwa inapata kigugumizi katika kuweka wazi baadhi ya mikataba kwa 
kile kinachodaiwa kuwa ni siri baina ya mwekezaji na serikali jambo 
ambalo halina ukweli tofauti na rushwa.
“Mimi nimekuwa nikifanya tafiti 
mbalimbali hasa za mausuala ya kukua kwa uchumi ni wazi kuwa zipo fedha 
nyingi ambazo zinapotea ambapo mwanzo wake unaanzia kwenye uingia ji wa 
mikataba hadi katika utekelezaji  ambazo zinaelekezwa katika rushwa”, 
alisema Mushi.
Mwahadhiri huyo wa UDSM alisema 
kuonyesha kuwa serikali haina dhamira ya kuondoa hiyo changamoto imekuwa
 ikiwaruhusu wawekezaji hao kutoweka hata akaunti zao wazi kama ilivyo 
kwa nchi zingine duniani.
Profesa Mushi ambaye pia aliwahi
 kuwa mshauri wa masauala ya uchimi wa Rais wa Zanzibar Abeid Aman 
Karume pamoja na Ofisi ya Hazina ya Tanzania alisema iwapo Tanzania 
itajikita katika uwazi, uwajibikaji na uadilifu maendeleo yatapatikana 
kwa haraka.
Mchumi huyo mwandamizi alisema 
ni dhahiri kuwa kumekuwepo kwa ukiukwaji mkubwa katika maamuzi hivyo ni 
vema kujiangalia upya kwa lengo la kuleta mabadiliko chanya kwa maslahi 
ya Taifa.
Alisema Tanzania ni nchi ambayo 
imebarikiwa fursa mbalimbali ila kukosekana kwa uadilifu na uwazi kwa 
baadhi ya watendaji rasilmali hizo zipo hatarini kupotea.
Dup(2)MREMBO.jpg)

No comments:
Post a Comment