TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, September 26, 2014

JAMII ITII SHERIA BILA SHURUTI

images
Na Benedict Liwenga, Maelezo-DSM.
 
Katika maisha ya kila siku, mwananchi anapaswa kutambua wajibu wake katika jamii ikiwa ni pamoja na kutii Sheria bila shuruti.
Katika maisha ya sasa nchini kumekuwa na vitendo vya ukiukwaji wa Sheria katika jamii na jamii imekuwa ikihusika katika matendo makubwa ya kijinai ambayo ni kinyume na sheria.
Hali hii imekuwa ikitokana na aidha jamii kutojua sheria, na muda mwingine ni kupuuzia tu maagizo na sheria mbalimbali.
Siku za hivi karibuni kumekuwepo na ukatili mkubwa ukitendeka katika jamii kwa kutokea kwa mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi ambapo wasiojua nini maana ya utu kwa makusudi wanakatiza uhai wa maisha ya binadamu wenzao na wengine kuwakata baadhi ya viungo vyao kwa tamaa ya kujipatia fedha pamoja na imani za kishirikina.
 
Jamii sio tu inaelewa kuwa kumdhuru mtu ni kosa la jinai bali pia jamii inatambua kuwa kuua pia ni kosa kubwa la jinai ambapo katika Sheria ya Kanuni ya adhabu Sura ya 16 kifungu cha 197 kimeeleza jinsi ambavyo kosa la kuua kwa kukusudia linamgharimu mtu adhabu ya kifo, lakini licha kuwepo kwa sheria hiyo, bado jamii inajihusisha na makosa ya kuua kila kukicha.
 
Katika mikoa ya Kanda ya Ziwa Victoria, suala la mauaji ya watu wenye Ulemavu wa Albino limekuwa ni tatizo kubwa kwani mauaji haya yanafanyika katika mazingira tu ya watu kuwa na imani potofu za kuukwaa utajiri wa haraka haraka.
 
Wakili wa kujitegemea Bwana Edwin Webiro anaeleza kuwa watu wengi wanafahamu kuwa kuua ni kosa kubwa lenye adhabu ya kifo ama kifungo cha maisha, bado watu hao hawajali juu ya uwepo wa Sheria ya kunyonga kwasababu wamekuwa wakiiona haitekelezwi ipasavyo, jambo linalowafanya wao waone ni haki kwao kufanya unyama wowote kwa watu wasio na hatia (watu wenye ulemavu).
 
Katika hali nyingine jamii pia imekuwa ikikiuka Sheria na kusababisha madhara makubwa pale ambapo ajari nyingi zimekuwa zikitokea mfululizo hivi karibuni na kusababisha vifo na kuacha ulemavu wa kudumu wa jamii.
 
Ajali hizi zimekuwa zikisababishwa na uzembe wa baadhi ya madereva wa mabasi pamoja na magari madogo kwani kumekuwa na ukiukwaji wa Sheria za barabarani ambapo kwa makusudi madereva hao wamekuwa wakikiuka sheria mbalimbali na kufanya mambo yanayosabisha ajari.
 

No comments:

Post a Comment