WAZIRI
 MKUU Mizengo Pinda amesema Serikali haitataifisha shule, zahanati, 
hospitali wala Vyuo Vikuu vinavyoendeshwa na taasisi za kidini na 
amewahimiza wajenge zaidi na zaidi ili kuisaidia jamii kubwa ya 
Watanzania.
Ametoa
 wito huo wakati akizungumza na walimu, wazazi na wahitimu wa kidato cha
 nne wa shule ya sekondari Magnificat iliyoko Sanya Juu, wilayani Siha 
mkoani Kilimanjaro.
Waziri
 Mkuu ambaye aliwasili Sanya Juu jana asubuhi (Jumamosi, Septemba 20, 
2014) akitokea Dodoma, alisema huko nyuma Serikali ilitaifisha shule na 
vyuo lakini kwa kiasi fulani ilishindwa kuviendesha ikaamua kuvirudisha 
kwa wamiliki wake ambao ni taasisi za kidini.
“Ni 
kweli huko nyuma tulikuwa navyo, lakini tumevirudisha kwenu tunataka na 
ninyi ni washirika katika kuleta maendeleo kwa wananchi walio wengi,” 
alisema Waziri Mkuu.
“Nilishawahi
 kusema huko nyuma na leo nasisitiza tena kwamba hatutaifisha shule, 
zahanati, hospitali wala Chuo Kikuu chochote cha taasisi ya kidini. 
Ninawasihi mjenge zaidi na zaidi,” aliongeza.
Waziri
 Mkuu ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa shule hiyo 
iliyoanzishwa Januari 15, 2011, aliwakabidhi vyeti wanafunzi 42 wa 
kidato cha nne wanaotarajia kufanya mtihani wa kidato cha nne Novemba, 
mwaka huu ikiwa ni mara ya kwanza kwa shule ya sekondari ya Magnificat 
kufanya mtihani huo.
Waziri
 Mkuu aliwapongeza wanafunzi hao kwa kushika nafasi ya kwanzawilayani 
Siha kwenye mitihani ya utamirifu (yaani mock) katika kidato cha nne. 
“Vilevile, shule hii imekuwa ya 12 kati ya shule 316 za Mkoa wa 
Kilimanjaro na ya 16 kati ya shule 564 kwa Kanda ya Kaskazini Mashariki 
zilizofanya mtihani huo. Mimi napata imani kuwa watafanya vizuri kwenye 
mtihani wao wa kidato cha nne Novemba 2014,” aliongeza.
Mapema,Mkuu
 wa Shirika la Masista la Kazi ya Roho Mtakatifu na Meneja wa Shule 
hiyo, Sista Inviolata Kessy alisema shule hiuo ilianzishwa kwa lengo la 
kutoa elimu bora na kuwashawishi watoto wa kike wa Kimasai waone umuhimu
 wa elimu na hivyo kuwaepusha na ndoa za utotoni. Vile vile, kuwapa 
msingi mzuri wa elimu kama sehemu ya maandalizi yao ya kupata elimu ya 
juu.
Alisema
 shule hiyo ambayo ni ya mchanganyiko na ya mchepuo wa sayansi na 
biashara, imefanikiwa kujenga maabara tatu za kemia, fizikia na 
baiolojia pamoja na chumba cha kompyuta.
Akisomarisalakwa
 niaba ya wahitimu, Anastazia Kimaro alisema shule hiyo inakabiliwa na 
changamoto nyingi zikiwemo ukosefu wa jengo la utawala pamoja na basi la
 shule la kuwapeleka wananfunzi kwenye ziara za mafunzo.
Aliomba
 pia wawe wanapelekewa magazeti ya kila siku na kila wiki ili wanafunzi 
wa shule waweze kupata taarifa mbalimbali za mambo yanayojiri nchini na 
duniani.
No comments:
Post a Comment