Kipimo Abdallah
CHAMA
 cha NCCR-Mageuzi kimesikitishwa na kitendo cha Bunge Maalum la Katiba 
kuhitaji wajumbe ambao hawapo nchini au ndani ya Bunge kuruhusiwa kupiga
 kura wakati ukweli ni kwamba ushiriki wao katika utengenezaji wa rasimu
 hiyo ulikuwa mdogo.
Hayo
 yamesemwa na Kaimu Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi Faustin Sungura wakati 
akizungumza na mwandishi wa habari hii jana jijini Dar es Salaam kwa 
njia ya simu.
Alisema
 utaratibu huo wa kuruhusu wajumbe walioko nje kupiga kura haujawahi 
kutokea katika Bunge lolote hapa duniani jambo ambalo linatia aibu kwa 
Taifa.
Kaimu
 Katibu huyo alisema iwapo wajumbe hao ambao hawakushiriki katika 
mchakato kwa kiwango cha kuridhisha wataruhusiwa kupiga kura hali hiyo 
ingekuwa hata kwa wale wa UKAWA kwani uwepo wao nje una sababu kama hao 
wengine.
“Jamani
 Watanzania tuamke hii sasa aibu tunapopelekwa pabaya haiwezekani watu 
wapo nje ya Bunge alafu wapewe nafasi ya  kupiga kura jambo ambalo 
haliwezi kuvumiliwa kwani linatia aibu nchi”, alisema.
Alisema
 katika Bunge hilo linaloendelea mkoani Dodoma mambo mengi yamekiukwa 
ila hapo walipofikia ni vema jamii ya Kitanzania ikafungua macho na 
kuamua kufanya maamuzi mazito kwani kinachoonekana ni watu kuhitaji kwa 
maslahi yao.
Sungura
 alisema ni vema Wabunge waliopo Dodoma wakatambua kuwa mambo megine 
hayalazimishwi kwani yanahusu jamii kubwa na sio kama wanavyofikiria 
kuwa wao ndio wanahusika pekee.
Alisema
 NCCR-Mageuzi imejipanaga kuhakikisha kuwa katiba hiyo inakataliwa 
kutokana na ukweli kuwa kilichopo ndani sio yaliyokuwa mapendekezo ya 
wananchi ambayo yaliwakilishwa na iliyokuwa Tume ya Katiba.
Sungura
 alisema ukweli dhidi ya UKAWA kutoka Bungeni umedhihirika hivyo juhudi 
zao ni kuhakikisha kuwa rasimu hiyo haipitishwi na wananchi kutokana na 
kudharauliwa kwa maoni yao ambayo walipendekeza katika rasimu ya Jaji 
Joseph Warioba.
 Kaimu
 Katibu Mkuu huyo alisema nguvu yao pia inaongezwa na maamuzi ya 
Mahakama Kuu hivi karibuni ambapo imeweka bayana kuwa kitendo 
kilichofanywa na Mwenyekiti wa Bunge hilo kupokea maoni mapya ni 
ukiukwaji wa sheria.
Sungura
 alisema mabadiliko na maingizo mapya yaliyofanywa na Bunge hilo ambalo 
alilitaja kuwa ni la upande mmoja yamekiuka sheria kwa kiwango kikubwa 
na cha kusikitisha.
Alisema
 kwa sasa NCCR- Mageuzi ipo katika mikakati ya kuhakikisha wananchi 
wanapata elimu sahihi juu ya mchezo mchafu unaofanywa na Bunge hilo 
jambo ambalo litawajengea uwezo wa kufanya maamuzi sahihi katika upigaji
 kura.

No comments:
Post a Comment