Afisa
 Habari wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Bi. Bestina Magutu
 akiwaeleza waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu kukamilika kwa 
maboresho ya kituo cha Mawasiliano ya Radio kwa ajili ya usafiri wa anga
 kilichopo Mnyusi mkoani Tanga, kilichojengwa na kampuni ya JATRON ya 
Norway, wakati wa Mkutano Uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari 
(MAELEZO) leo Jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Mhandisi Mkuu toka Mamlaka
 Hiyo Bi. Valentine Kayombo.
Mhandishi
 Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Bi. Valentine 
Kayombo akiwaeleza waandishi wa Habari(Hawapo pichani) faida 
zitakazopatikana kutokana na kukamilika kwa Kituo hicho ikiwamo kuongeza
 ufanisi wa utoaji huduma za uongozaji ndege, wakati wa Mkutano 
Uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari(MAELEZO) leo Jijini Dar es 
Salaam.Kulia ni Afisa Habari wa Mamlaka Hiyo Bi. Bestina Magutu. 
Inspeka
 Mwandamizi Idara ya Udhibiti Usalama wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga 
Tanzania (TCAA) Bw. Redemptus Bugumula akiwaeleza waandishi wa habari 
kuhusu ongezeko la marubani wanawake nchini ambao wanafikia Takribani 
Kumi kwa sasa wakati wa Mkutano Uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya 
Habari (MAELEZO) leo Jijini Dar es Salaam.Kulia ni Mhandisi Mkuu toka 
Mamlaka Hiyo Bi.Valentine Kayombo.
Mamlaka ya Usafiri wa Anga 
Tanzania (TCAA) imekamilisha mradi wa kuboresha kituo cha kupokea na 
kutuma mawasiliano ya radio zinazotumika katika usafiri wa anga 
kilichoko Mnyuzi mkoani Tanga.
Mradi huo uliojengwa na kampuni ya
 JOTRON ya NORWAY umegharimu Serikali zaidi ya shilingi milioni 200 na 
ulikabidhiwa rasmi kwa TCAA mapema mwezi Agosti mwaka huu.
Hayo yamesemwa na Afisa Habari wa 
Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Bi. Bestina Magutu wakati wa 
mkutano na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam.
Magutu alisema kuwa kukamilika kwa
 kituo hicho kumeongeza ufanisi wa utoaji huduma za uongozaji ndege na 
kuimarisha zaidi usalama wa safari za anga hapa nchini.
Akifafanua zaidi Magutu amesema 
hali hiyo itachangia kuongezeka kwa mapato ya Mamlaka hiyo yanayotokana 
na tozo la huduma za uongozaji ndege.
Akizungumzia mikakati ya Mamlaka 
hiyo Magutu amesema inaendelea kuwekeza katika miundo mbinu ya kuongozea
 ndege hivyo kwenda sanjari na mabadiliko ya teknolojia pamoja na kumudu
 ukuaji wa Sekta ya usafiri wa anga hapa nchini.
Katika hatua nyingine Mamlaka hiyo
 imesema kuwa wanafunzi watano waliopewa ufadhili wa kusomea urubani 
nchini Afrika ya Kusini wameendelea kupata ufaulu wa juu na kushika 
nafasi ya kwanza hadi ya tano katika darasa la watu 14 katika shule ya 
urubani nchini Afrika ya Kusini.
Takwimu za mwaka 2013 zinaonyesha 
ongezeko la miruko ya ndege ( flight movements) kutoka 222,430 mwaka 
2012 hadi kufikia miruko 230,458 sawa na ongezeko la asilimia 3.6 
kadhalika katika kipindi hicho idadi ya abiria imeongezeka kutoka 
4,056,925 hadi kufikia 4,626,016 sawa na ongezeko la asilimia 14.Idadi 
ya abiria inatarajiwa kufika zaidi ya milioni 5 kufikia mwishoni mwa 
mwaka 2014.
No comments:
Post a Comment