KAMPUNI YA PLATINUM YATOA MSAADA WA VIFAA VYA MICHEZO KWA AJILI YA SHIMIWI.
 
           
       
       
       
         
       
       
        
 Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni ya Platinum Credit Ltd Bw. Elias Samwel 
akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi msaada wa vifaa vya 
michezo kwa baadhi ya Timu za Wizara na Taasisi za Serikali leoj jijini 
Dar es Salaam, vifaa hivyo vimetolewa ili kusaidia timu hizo 
zinazoshiriki mashindano ya SHIMIWI ambayo mwaka huu yanatarajiwa 
kufanyika kuanzia tarehe 27 Septemba hadi tarehe 11 Oktoba mkoani 
Morogoro.Kulia ni Kaimu Katibu Mkuu wa SHIMIWI Moshi Makuka.
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Sihaba 
Nkinga akimtunuku cheti Mwakilishi wa Platinum Credit Ltd Bw. Ferdinand 
Kambanyumba ikiwa ni kutambua na kuthamini mchango wao katika kuendeleza
 michezo wakati wa hafla ya kuwaaga wachezaji wa Wizara watakaoshiriki 
mashindano ya SHIMIWI 2014 

 
Kaimu
 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Habari, Vijana,
 Utamaduni na Michezo Bibi. Concilia Niyibitanga akipokea kwa niaba ya 
Katibu Mkuu, msaada wa vifaa vya michezo kutoka kwa Meneja Mauzo wa 
Kampuni ya Platinum Credit Ltd Bw. Ferdinand Kambanyuma wakati wa hafla 
ya kukabidhi msaada huo kwa baadhi ya timu za Wizara na Taasisi za 
Serikali zinazotarajia kushiriki mashindano ya SHIMIWI leo jijini Dar es
 Salaam.Mashindano hayo yanatarajiwa kuanza rasmi kuanzia tarehe 27 
mwezi huu na kumalizika tarehe 11 Oktoba mkoani Morogoro.
Kaimu
 Katibu Mkuu wa SHIMIWI Bw. Moshi Makuka (kulia) akipokea msaada wa 
vifaa vya michezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni ya Platinum 
Credit Ltd Bw. Elias Samwel wakati wa hafla ya kukabidhi msaada huo kwa 
baadhi ya timu za Wizara na Taasisi za Serikali zinazotarajia kushiriki 
mashindano ya SHIMIWI leo jijini Dar es Salaam.Mashindano hayo 
yanatarajiwa kuanza rasmi kuanzia tarehe 27 mwezi huu na kumalizika 
tarehe 11 Oktoba mkoani Morogoro.
Mwenyekiti
 Timu ya Utumishi Bw. Lumuli Mtaki (kushoto) akipokea msaada wa vifaa 
vya michezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni ya Platinum Credit
 Ltd Bw. Elias Samwel wakati wa hafla ya kukabidhi msaada huo kwa baadhi
 ya timu za Wizara na Taasisi za Serikali zinazotarajia kushiriki 
mashindano ya SHIMIWI leo jijini Dar es Salaam.Mashindano hayo 
yanatarajiwa kuanza rasmi kuanzia tarehe 27 mwezi huu na kumalizika 
tarehe 11 Oktoba mkoani Morogoro. 
 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment