TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, September 26, 2014

TIMU YA TAIFA YA KARATE TANZANIA YAJIANDAA KWENDA ALBANIA KUSHIRIKI MASHINDANO YA DUNIA.

 Rais wa Shirikisho la Dunia la mchezo wa Karate (UPAM), Profesa  Martina Maurizio (kulia), akiwaelekeza jambo wachezaji wa mchezo huo walioko kambini Dar es Salaam jana. Wachezaji sita wa timu hiyo wanatarajia kuondoka Septemba 28 mwaka huu kwenda nchini Albania kushiriki mashindano ya dunia ya mchezo huo.
Wachezaji hao sita wakiwa wameshika bendera ya timu hiyo. Kulia ni  Rais wa Shirikisho la Dunia la mchezo wa Karate (UPAM), Profesa  Martina Maurizio.
Katibu Mkuu wa Chama cha Wataalamu wa Tiba za Michezo Tanzania (TASMA). Dk. Nassoro Matuzya (kushoto), akimpima uzito mchezaji, Ramadhan Jangle ikiwa ni maandalizi ya mashindano hayo. 
 Dk. Nassoro Matuzya (kushoto), akimpima presha mchezaji, Heri Msukile. (Imeandaliwa na mtandao wa habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
Mwalimu wa mchezo huo, Max (kulia), akimfua Master Dhabiti Athuman Msawila. ‘Master Hugu’ 
 Mchezaji Ramadhan Hassan (kulia), akikwepa kwanja la Heridini Mwinyiheri wakati wakiendelea na mazoezi katika Klabu ya Yanga Jangwani jana.
Wachezaji Hamisi Magigo (kushoto) na Master Dhabiti Athuman Msawila. ‘Master Hugu’  wakirushia makonde katika mazoezi hayo.
 
Dotto Mwaibale
 
WACHEZAJI sita wa timu ya  Karate wanatarajia kuondoka nchini kwenda Albania kushiriki mashindano ya dunia ya mchezo huo.
Washiriki hao tayari wamefanyiwa vipimo vya afya zao pamoja na uzito Dar es Salaam jana na Dk. Nassoro Matuzya ambaye ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wataalamu wa Tiba za Michezo Tanzania (TASMA).
Kikosi hicho cha watu 20 kinatarajiwa kuondoka nchini Septemba 28 kuelekea nchini humo kwa mashindano hayo.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Rais wa Shirikisho la Dunia la mchezo huo (UPAM) Profesa  Martina Maurizio alisema wachezaji hao wataungana  wataungana na wenzao kutoka Mwanza, Unguja na Arusha ambapo utafanyika mchujo ili kupata timu ya taifa.
Alisema wachezaji hao wapo kambini  na wamepata mafunzo ya kutosha na hivyo ni lazima warudi na ushindi pamoja na kuitangaza Tanzania duniani.
“Watanzania wengi bado hawajaupa kipaumbele mchezo huu jambo linalofanya usahaulike lakini watajitahidi kuufanya mchezo huo ukubalike hapa nchini kama ilivyo kwa nchi nyingine.
Maurizio alimpongeza Mkurugenzi wa Princecasino kwa kujitolea kwa hali na mali kudhamini safari hiyo.

No comments:

Post a Comment